• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

TASAF

  • UTANGULIZI:

Halmashauri ya Wilaya ya Songea inatekeleza Mpango huu wa kunusuru kaya maskini awamu ya tatu kipindi cha pili  na ulianza kutekelezwa rasmi mnamo February  2020.

 Lengo la mpango huu wa kunusuru kaya maskini ni kuwezesha kaya maskini kuongeza kipato, fursa na uwezo wa kugharimia mahitaji muhimu kwa kupitia vikundi vya kuweka na kuwekeza vya walengwa, kusaidia kaya maskini za wazee, watoto waliojiandikisha shule na wale walio chini ya miaka mitano na kaya za watu wenye ulemavu.


  • SHUGHULI ZINAZOTEKELEZWA: 

2.0.1. UTOAJI WA RUZUKU KWA WALENGWA.

Halmashauri ya Wilaya ya songea imeanza utekelezaji wa mpango huu kunusuru kaya maskini mnamo mwaka 2015 kwa kutoa ruzuku  ya TASAF kwa walengwa  waapatao 5,257 kutoka katika vijiji 56.

2.0.2 MIRADI YA KUTOA AJIRA YA MUDA KWA WALENGWA

Halmashauri ya wilaya ya songea inatekeleza miradi ya kutoa ajira ya muda kwa walengwa, mirdi hii huibuliwa na wananchi kupitia mikutano maalum ya vijiji ya wananchi wote na hutekelezwa na walengwa wa mpango kwa lengo la kuongeza kipato kwa kaya.

Miradi hii hutekelezwa Zaidi kipindi cha ARI, ni kipindi ambacho kinakuwa kigumu kwa walengwa kupata mahitaji yao inavyotakiwa. Kwa halmashauri ya wilaya ya songea hutekeleza miradi hiyo kuanzia mwezi Sept kila mwaka na hukamilika mwezi februari kila mwaka.

Mpango huu wa utekelezaji wa miradi ya kutoa ajira ya muda kwa walengwa ni wa kipindi cha miezi sita (6) na kila mwezi  walengwa hufanya kazi siku kumi, kwa masaa manne tu kila siku, na hulipwa shilingi 3,000 kila siku ambayo mlengwa atafanya kazi.

Miradi hii hutekelezwa kila kijiji na aina miradi inayotekelezwa ni ujenzi wa vivuko vya watembea kwa miguu, uboreshaji wa visima vya asili, uboreshaji wa barabara za mashambani, uanzishwaji wa mashamba ya korosho, uanzishwaji wa mashamba ya parachichi na utengenezaji wa pavement block ambazo zimewekwa kwenye sekondari na zahanati.

2.0.3. MIRADI YA  UJENZI WA MIUNDO MBINU MBALIMBALI

Halmashauri ya wilaya ya songea imetekkeleza na inatekeleza miradi ya ujenzi wa miundo mbinu mbalimbali nayo ni kama ifuatavyo;

  • Mradi wa ujenzi wa soko, vyoo matundu 6 na vizimba 82 katika kijiji cha Peramiho ambao imetumika takribalin shilingi milioni 185. Ujenzi umekamilika na unatumika.
  • Ujezni wa nyumba ya mtumishi katika hospitali ya wilaya kijiji cha Mpitimbi B ambayo imetumia jumla ya shilingi milioni 68. Ujenzi umekamilika na unatumika.
  • Ujenzi wa nyumba mbili za watumishi, ujenzi wa vyoo matundu 6 na uchimbaji wa kisima kirefu katika zahanati ya kijiji cha mdunduwalo ambayo imetumika jumla ya shilingi 154. Ujenzi umakamilika na unatumika.
  • Ujenzi wa kituo cha  magari, vyoo matundu 6, vibanda vya mlinzi 2, jengo la utawala 1, ujenzi wa  maduka 32 na ujenzi wa uzio katika kijiji cha Parangu. Fedha zilizopokelewa kwa ajili ya ujenzi ni milioni 202. Ujenzi unaendelea.
  • Ujenzi wa kituo cha magari, vyoo matundu 6, vibanda vya mlinzi 2, jengo la utawala 1, maduka 36 na ujenzi wa uzio katika kijiji cha lundusi. Fedha zilizopokelewa kwa ajili ya ujenzi ni milioni 434. Ujenzi unaendelea.

2.0.4 MPANGO WA UWEZESHWAJI KIUCHUMI WALENGWA (PRODUCTIVE GRANT)

Halmashauri ya wilaya ya songea inatekeleza mpango katika vijiji 36 kati ya vijiji 56. Mpango huu TASAF inawapa walengwa wenye uwezo wa kufanya kazi ruzuku ya uwezeshwaji  kiuchumi kiasi cha 350,000 kila mlengwa kwa ajili ya kuanzisha miradi mbalimbali. Katika halmashauri ya wilaya ya songea jumla ya walengwa 1,676 wamepewa ruzuku hii na wameanzisha shughuli za uzalishaji za ufugaji wa kuku, mbuzi, nguruwe, mama lishe na kilimo cha mbogamboga.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • WASIRA ATIA NENO UKAMILISHAJI WA MIRADI SONGEA DC, AMPONGEZA DKT. SAMIA

    June 12, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA SONGEA AWAPONGEZA WATENDAJI WA HALMASHAURI KWA KUSIMAMIA VIZURI UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA LISHE BORA

    June 11, 2025
  • MATUMIZI YA LISHE ILIYO BORA YASISITIZWA MASHULENI

    June 10, 2025
  • KITUO CHA AFYA MATIMILA CHAKABIDHIWA GALI LA WAGONJWA.

    June 06, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa