• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

DC NDILE AIPONGEZA HALMASHAURI YA SONGEA KWA KUIMARISHA HALI YA LISHE, ATOA WITO WA KUENDELEZA JITIHADA

Tarehe ya Kuwekwa: November 17th, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mheshimiwa Kapenjama Ndile, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa hatua kubwa zinazochukuliwa kuboresha lishe katika jamii kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2025/2026 (Julai–Septemba). Ametoa pongezi hizo leo, 17 Novemba 2025, wakati wa kikao cha lishe kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Ndile ameisisitiza Halmashauri kuendeleza ari ya kuhakikisha makundi yote ndani ya jamii, ikiwemo watoto, kina mama wajawazito, vijana na wazee, yanapata lishe bora na stahiki. Amesema kuwa mafanikio ya lishe hayapaswi kuwa ya msimu, bali yawe endelevu ili Songea iendelee kuwa mfano bora katika juhudi za kupambana na utapiamlo nchini.

Aidha, amewataka wataalamu wa afya katika vituo mbalimbali kuimarisha ufuatiliaji wa taarifa za afya za watoto kwa kupima urefu, uzito na hali ya ukondefu mara kwa mara, hatua itakayochangia kubaini changamoto mapema na kuongeza ufanisi wa huduma za lishe.

Katika uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa afua za lishe, Bi. Joyce Sipira, Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, alieleza kuwa hali ya lishe inaendelea kuimarika. Amesema kuwa shule nyingi sasa zinatoa chakula kwa wanafunzi, jambo ambalo limepunguza utoro wa wanafunzi shuleni.

Pia alibainisha kuwa idadi ya mashine za kusagia unga wenye virutubishi imeongezeka kutoka 5 hadi 8, hatua ambayo imeongeza upatikanaji wa unga ulioimarishwa kiafya katika jamii—hatua muhimu katika kupambana na udumavu na upungufu wa virutubisho mwilini.

Mhe. Ndile amewataka watendaji wa kata kuhakikisha mashine hizo mpya zinatangazwa na kufahamika katika vijiji vyote ili kuongeza matumizi na kuwafikia wananchi wengi zaidi. Katika hatua nyingine za kikao hicho, alikabidhi kibao maalum cha upimaji urefu wa watoto, lengo likiwa ni kuimarisha ufuatiliaji wa ukuaji na afya ya watoto katika ngazi ya jamii.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • FAHAMU KUHUSU BARAZA LA MADIWANI; MUUNDO NA UTENDAJIKAZI WAKE

    November 25, 2025
  • SONGEA DC, YATEMBELEA MIKOA INAYOLIMA KAHAWA KWA LENGO LA KUPATA UZOEFU

    November 19, 2025
  • DC NDILE AIPONGEZA HALMASHAURI YA SONGEA KWA KUIMARISHA HALI YA LISHE, ATOA WITO WA KUENDELEZA JITIHADA

    November 17, 2025
  • SONGEA DC YAPOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA TSH MILIONI 30 KITUO CHA AFYA MUHUKURU LILAHI

    November 20, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa