• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

FAHAMU KUHUSU BARAZA LA MADIWANI; MUUNDO NA UTENDAJIKAZI WAKE

Tarehe ya Kuwekwa: November 25th, 2025


Baraza la Madiwani ni chombo muhimu katika uendeshaji wa mamlaka za Serikali za Mitaa, Ndilo linalowakilisha wananchi katika ngazi ya Halmashauri, na kupitia Baraza hili, maamuzi mbalimbali ya kimkakati na kimaendeleo hupitishwa. Madiwani wanaounda baraza ni wale waliochaguliwa na wananchi pamoja na wale wa viti maalum.

Kitengo cha mwasiliano Serikalini, kilifika Ofisi ya Utumushi Halmashauri ya Wilaya ya Songea na kuongea na Mkuu wa Idara hiyo Ndg. Idd Kalingonji ambapo ameeleza Lengo kubwa la kuwa na Baraza la madiwani ni kurejeshwa kwa mhimili wa ngazi ya kiutawala katika Serikali za Mitaa ambapo huukamilisha muundo wa kimaamuzi na usimamizi katika Halmashauri.

Katika kipindi hiki ambacho Halmashauri huunda Baraza jipya la madiwani, kuna hatua muhimu zinazofanyika. Moja ya hatua hizo ni uchaguzi wa Mwenyekiti wa Halmashauri, ambaye ndiye kiongozi mkuu wa kisiasa katika baraza hilo, Mwenyekiti huyo huchaguliwa na madiwani wenyewe kupitia kikao cha kwanza cha baraza.

Katika mchakato wa kumpata mwenyekiti wa Halmashauri chama chochote cha siasa chenye mwakilishi kinaweza kupendekeza jina na kuliwasilisha kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri na kuweza kupigiwa kura na wajumbe wote.

Mwenyekiti wa Halmashauri ana majukumu ya kuongoza vikao vya Baraza, kusimamia utekelezaji wa maamuzi ya Baraza, kuhakikisha uwajibikaji, na kuwa kiunganishi kati ya Baraza na Wataalamu wa Halmashauri kwa pamoja, Baraza na menejimenti ya Halmashauri hushirikiana kupanga, kusimamia na kufuatilia miradi mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yao.

Hivyo Baraza la Madiwani hufanya maamuzi ya mwisho kuhusu Halmashauri kama vile fedha, miradi, mipango na manunuzi ambapo hufanywa na kamati za kudumu kama vile Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango, Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira na Kamati ya Elimu, Afya na Maji. Pia kuna kamati zisizo za kudumu ambazo ni Kamati ya Maadili ya Madiwani na Kamati ya kudhibiti UKIMWI.

Kwa ujumla kikao cha baraza la madiwani kinahudhuriwa na madiwani wote wa kuchaguliwa na wa viti maalum, wakuu wa Idara na vitengo ( wataalam ), waalikwa kama vile Mkuu wa Mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya na Katibu Tawala wa Wilaya, Ofisi ya Ufuatiliaji na usimamizi wa Serikali za Mitaa pia kamati ya ulinzi na usalama, viongozi wa vyama, wananchi na waandishi wa habari.

Katika kuelekea kuundwa kwa Baraza jipya la madiwani Ndug Idd Kalingonji Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea amesema Halmashauri imejipanga kikamilifu ikiwemo uandaaji wa taarifa za utendaji kazi wa Halmashauri kwa kipindi chote ambacho Baraza halikuwepo, kumuandaa Hakimu kwaajili ya Kiapo cha madiwani, kiapo cha Maadili na kiapo cha tamko mbele ya Mkurugenzi.

Pia Halmashauri imeandaa vitendea kazi kwaajili ya uchaguzi wa Mwenyekiti wa Halmashauri kama vile masanduku (Ballot paper) kuandaa mazingira rafiki ya kupigia kura, sare za wajumbe pamoja kuuandaa ukumbi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • FAHAMU KUHUSU BARAZA LA MADIWANI; MUUNDO NA UTENDAJIKAZI WAKE

    November 25, 2025
  • SONGEA DC, YATEMBELEA MIKOA INAYOLIMA KAHAWA KWA LENGO LA KUPATA UZOEFU

    November 19, 2025
  • DC NDILE AIPONGEZA HALMASHAURI YA SONGEA KWA KUIMARISHA HALI YA LISHE, ATOA WITO WA KUENDELEZA JITIHADA

    November 17, 2025
  • SONGEA DC YAPOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA TSH MILIONI 30 KITUO CHA AFYA MUHUKURU LILAHI

    November 20, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa