• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SONGEA DC YAHAMASISHA UMUHIMU WA LISHE BORA KWA WATOTO SHULENI

Tarehe ya Kuwekwa: November 27th, 2025


Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea kupitia Kitengo cha Mifugo, ikiongozwa na Bw. Anton Sekumbo, imeendesha zoezi maalum la uhamasisho wa ulaji wa lishe bora kwa wanafunzi kwa kugawa maziwa mashuleni leo Novemba 27, 2025. Hatua hii ni sehemu ya jitihada endelevu za Serikali kuhakikisha watoto wanakuwa na afya bora na miili imara kupitia ulaji wa vyakula vyenye virutubishi muhimu.


Kwa mujibu wa wataalamu hao, Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ni miongoni mwa idara mtambuka zinazoshirikiana kwa karibu na Idara ya Afya katika kutekeleza masuala ya lishe kwa watoto, hususan wale wa umri wa shule. Kupitia ziara hiyo, wataalamu walipata nafasi ya kutoa elimu kwa wanafunzi na walimu juu ya faida za unywaji wa maziwa mara kwa mara, wakibainisha kuwa maziwa yana virutubishi muhimu vinavyosaidia ukuaji wa mwili, uimarishaji wa mifupa, kuongeza kinga ya mwili na kuchangia uwezo wa mwanafunzi kujifunza kwa ufanisi.

Aidha, program ya ugawaji wa maziwa mashuleni inalenga kuwajengea wanafunzi tabia ya kunywa maziwa si tu wakiwa shuleni bali pia majumbani, hivyo kuhakikisha afya njema inajengwa tangu utotoni. Zoezi hilo limefanyika katika shule za msingi Mapinduzi, Kilimani na Morogoro ambapo wanafunzi walionesha mwamko mkubwa na furaha wakati wa kupokea maziwa hayo. Elimu hiyo imeenda sambamba na kaulimbiu ya maadhimisho ya lishe ya mwaka 2025 isemayo: “Afya ni Mtaji Wako, Zingatia Unachokula.”

Vilevile, Kitengo cha Mifugo kimeendelea kutekeleza program mbalimbali za kuhamasisha ulaji wa vyakula vyenye protini, ambapo kitengo kiligawa sungura na mabanda ya kufugia sungura kwa shule mbalimbali kwa mwaka uliopita. Hatua hiyo ilikusudia kuchochea ufugaji wa sungura ili watoto na jamii kwa ujumla waweze kupata nyama, ambayo ni chanzo kizuri cha protini kwa ukuaji wa mwili.


Bw. Sekumbo alibainisha kuwa zoezi la leo ni mwendelezo wa kampeni pana ya lishe bora katika Halmashauri ya  Wilaya ya Songea, na litaendelea kufanyika mara kwa mara kwa lengo la kupunguza udumavu na kuongeza uelewa wa jamii kuhusu ulaji sahihi. Alisisitiza kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya mtoto kiakili na kimwili, hivyo ni wajibu wa wazazi, walimu na jamii kwa ujumla kuhakikisha watoto wanapata chakula chenye ubora.

Halmashauri ya Wilaya ya Songea imeendelea kuwa mfano wa kuigwa katika kutekeleza program za lishe, ikilenga kuandaa kizazi chenye afya bora na uwezo wa kuchangia maendeleo ya Taifa.


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SONGEA DC YAHAMASISHA UMUHIMU WA LISHE BORA KWA WATOTO SHULENI

    November 27, 2025
  • FAHAMU KUHUSU BARAZA LA MADIWANI; MUUNDO NA UTENDAJIKAZI WAKE

    November 25, 2025
  • SONGEA DC, YATEMBELEA MIKOA INAYOLIMA KAHAWA KWA LENGO LA KUPATA UZOEFU

    November 19, 2025
  • DC NDILE AIPONGEZA HALMASHAURI YA SONGEA KWA KUIMARISHA HALI YA LISHE, ATOA WITO WA KUENDELEZA JITIHADA

    November 17, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa