• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

ZIARA ya Mhe. Mkuu wa Wilaya ya kusikiliza na Kutatua kero za Wanachi.

Tarehe ya Kuwekwa: June 29th, 2023

MKUU wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Kapenjama Ndile amewataka Viongozi wa Kata, Vijiji na Vitongoji waweke utaratibu wa kusikiliza na kutatua kero za migogoro ya ardhi katika maeneo yao.

Ametoa kauli hiyo jana Juni 28, 2023 katika mkutano wa adhara uliofanyika katika    Kata ya Muhukuru Kijiji cha Nakawale ambapo lengo la mkutano huo ni kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kijiji hicho.

Katika ziara yake aliambatana na Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkurugenzi Mtendaji, kamati ya ulinzi na usalama Wilaya pamoja na timu ya Wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Akizungumza katika mkutano huo amewataka wananchi wote ambao wameuza ardhi za Kijiji pasipo kufuata taratibu na sheria warejeshe ardhi hizo katika Serikali ya Kijiji.

‘‘Ardhi ni mali ya Kijiji kitendo cha kuuza ardhi ni ulanguzi unaotokana na tamaa hivyo unawanyima haki vizazi vinavyokuja sasa watu wote mliouziana ardhi bila kufuata taratibu huo ni ubatili hizo ardhi zitarejeshwa katika Serikali ya Kijiji’’, amesisitiza Mhe. Ndile.

Aidha, Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ameongeza kuwa katika Kijiji cha Nakawale Serikali ya Kijiji haijawahi kutenga eneo la ufugaji ni eneo la kilimo hivyo kama kuna wafugaji wameingiza mifugo katika eneo hilo waiondoe.

Vilevile amesema ardhi ya Tanzania haiuzwi bali inamilikishwa kutoka kwa mtu mmoja Kwenda kwa mwingine hivyo kwa mwananchi yeyote anaetaka kumiliki ardhi ahakikishe anapeleka maombi katika ofisi ya Serikali ya Kijiji ili maombi yake yaweze kujadiliwa na sio kitendo cha kumilikishana bila kufuata taratibu.

Pia katika mkutano huo uliambatana na zoezi la kuunda tume yenye watu 11 kutoka katika kila Kitongoji kwa kushirikiana na wataalamu wa ardhi kutoka Halmashauri kufanya uchunguzi wa kina na kitaalamu wa migodoro hiyo na majibu kutolewa kwa muda watakaopewa.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa