• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Zao la ufuta lilivyowanufaisha wakulima Songea

Tarehe ya Kuwekwa: June 11th, 2020

WAKULIMA wa zao la ufuta katika Wilaya za Namtumbo,Songea na Tunduru mkoani Ruvuma wameanza kunufaika na zao hilo baada ya kupokea shilingi bilioni 16.8 tangu kuanza kuuza zao hilo kwa mfumo wa stakabadhi ghalani Apirili 30 mwaka huu.

Hayo yamesemwa na  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme  wakati anafungua kikao maalum Baraza la madiwani la Halmashauri ya Namtumbo cha kujadili Hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi  Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

“Mpaka sasa katika minada ya Songea,Namtumbo na Tunduru zimeuzwa kilo milioni 8.2 za zao la ufuta zilizosababisha wakulima kupata sh.bilioni 16.8 ambazo zitaendelea  kuongezeka kupitia minada inayokuja’’,alisisitiza Mndeme.

Mndeme amesema tangu kufunguliwa kwa mnada, vyama  vya ushirika AMCOS kupitia zao la ufuta vimekwishapata  zaidi ya sh.milioni 500 na ushuru uliopatikana kwenye vyama vikuu  vya ushirika SUNAMCO na TAMCO ni shilingi  milioni 2.48.

Amesisitiza kuwa  Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuonesha mafanikio makubwa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani na kwamba mfumo huo utaendelea kutumika kwenye mazao ya soya na Mbaazi ili  kulinda haki ya wakulima.

 Mndeme amesema  Mkoa wa Ruvuma msimu huu unatarajia kuendelea kuwa gwiji katika mazao ya chakula ambapo  mahitaji ya chakula katika Mkoa wa Ruvuma ni tani laki 3.38 hadi sasa Mkoa  una ziada ya chakula zaidi ya tani laki tisa.

Amesisitiza kuwa Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa inayofanya vizuri katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara nchini  na kwamba  hadi kufikia Mei 15 mwaka huu  zilikuwa zimevuna tani milioni  1.3.

Wakati huo huo Mndeme  amewapongeza Halmashauri ya Namtumbo kwa kupata hati safi ya ripoti ya CAG kwa miaka minne mfululizo kuanzia mwaka 2015/2016 hadi 2018/2019.

Mndeme amewapongeza Madiwani na watalaam kwa kuweza kuchangia asilimia 99.77 katika mfuko wa wanawake,wazee,vijana na watu wenye ulemavu na   kukusanya mapato ya ndani Zaidi ya Sh. bilioni 1.94 katika mwaka wa fedha wa  2018/2019.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa