• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

Tarehe ya Kuwekwa: July 1st, 2025

Wakazi wa Peramiho Wameanza Kunufaika na  Stend ya Kisasa  ambayo imezinduliwa Leo Julai Mosi 2025  na Kanali Ahmed Abbas Ahmed Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mradi wa Ujenzi wa Stend ya Kisasa Umetekelezwa kwa Kutumia Mfuko wa Maendeleo  ya Jamii (TASAF) Tanzania Social Action Fund  awamu ya Tatu Kwa Kushirikiana na Wananchi wa Kijiji Cha Lundusi, Zaidi ya Milioni 600 Zimetumika Kutekeleza Mradi huo.


Mkuu. wa Mkoa wa Ruvuma akizindua Stend hiyo ya Kisasa amewashukuru sana Watendaji wote wa TASAF, kwa Kazi nzuri Waliyoifanya kwa Kushirikiana na Wananchi Kuhakikisha Stend hiyo inakamilika ikiwa na Miundombinu yote Muhimu, nakuwataka Wananchi wa Peramiho Kumpatia Heshima anayostahili aliyekuwa Mbunge wa  Jimbo Hilo ambaye pia ni Waziri wa Afya Jenista Mhagama kwa Kupambania Upatikanaji wa Stend hiyo ya Kisasa akishirikiana bega kwa bega na Halmashauri ya Songea DC, akimshukuru pia Dkt.Samia  Kwa kutoa Fedha nyingi za Miradi Mkoani Ruvuma,pamoja nakuwashukuru Wananchi.

RC Kanali Ahmed Abbas Ahmed ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Songea wakiwemo Wananchi  wa Peramiho Kuitunza nakuilinda Miundombinu hiyo ya Stend, ili waendelee kupata Huduma iliyobora ya Usafiri Katika Mazingira Rafiki, Nakuwaagiza Mkuu wa Wilaya ya Songea Kapenjama Ndile na Mkurugenzi  Mtendaji wa Songea DC Bi. Elizabeth Gumbo kuhakikisha kunakuwa na Miundombinu ya Maji ya Uhakika kwa ajili ya Huduma ya Vyooni na Matumizi ya Maji kwa abiria, Madereva na Watu Wote ambao Watatumia Stend hiyo ya Kisasa iliyosheheni Maduka , Ujenzi wa  Ofisi, Ujenzi wa Uzio.


Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Kutoka Makao Makuu Bwn. Shadrack Mziray ameishukuru Serikali ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna inavyopambania Watu kuondokana na Umaskini Kupitia  Miradi Mbalimbali ya Maendeleo ikiwemo  TASAF Kuwezesha Kaya Maskini katika Kuwaongezea Kipato na Fursa anuai za Kiuchumi, na tangu kuanzishwa kwa TASAF Mwaka 2000 Hadi kufikia sasa  Zaidi ya Shilingi Trillion 1  Kama Ruzuku zimewafikia  Walengwa hapa Nchini, akibainisha kwamba ifikapo Septemba 30 Mwaka huu Mradi huo Utahitimishwa Kote Nchini, ambapo Walengwa ambao hawajapokea Malipo Yao  Watalipwa Kabla ya Mwezi Sept, Lakini Mradi Mwingine Mpya Utaanza Mwezi Octoba Mwaka huu.


Wananchi wenyewe wanasema Ujenzi wa Stend ya Kisasa Peramiho Utawapunguzia aghali ya Usafiri, Wananchi wa Lundusi na Wale waishio Maeneo Jirani Hutumia Shilingi 1500 Hadi 2000 Kutoka Hospital ya Mtakatifu Joseph  Peramiho Hadi  Kufika Kijiji Cha Lundusi na Zilipo Ofisi za Halmashauri ya Songea DC, Ikilinganishwa na Nauli ya 1200 Kutoka Songea Mjini Hadi Kufika Peramiho, Wameishukuru sana TASAF na  Serikali ya Dkt. Samia, Wakimpa Heko na Jenista Mhagama Waziri wa Afya na Mbunge aliyemaliza muda wake.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

    July 01, 2025
  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2025

    June 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa