• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WIZARA YA KILIMO KUTOA USHIRIKIANO KULETA TIJA ZAO LA KAHAWA

Tarehe ya Kuwekwa: December 8th, 2023


Naibu Waziri wa kilimo David Ernest Silinde amesema  Wizara ya kilimo itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha ili kuleta tija katika kilimo cha kahawa wakati akizungumza kwenye mkutano wa  wadau wa kahawa Songea uliofanyika kwenye ukumbi wa  Halmashauri ya Manispaa ya Songea 06 Disemba 2023.

Pamoja na mambo mengineMhe  Naibu Waziri amesema zao la kahawa ni miongoni mwa mazao ya kimkakati nchini Tanzania ambalo linaliingizia fedha nyingi za kigeni hivyo Wizara ya kilimo imejipanga kikamilifu kusimamia vyema zao hilo. Amesema

“ Niseme kwamba Wizara ya kilimo tumejipanga vizuri hata kwenye zao hili la kahawa nyinyi nyote mnafahamu, zao la kahawa ni ,moja ya mazao ya kimkakati ya kibiashara tuliyonayo nchini ukiacha korosho, tumbaku, pamba na katani zao la kahawa ni miongoni mwa ,mazao makubwa nchini ambayo sisi kama Wizara tunalitegemea na ni zao ambalo linaingiza fedha nyingi za kigeni katika nchi yetu, kwahiyo niwaondoe shaka maamuzi na ubunifu ambao Mkuu wa Wilaya umeuleta kwa wananchi wako wa Halmashauri zako ni uamuzi unaoonekana  unalengo la ilani ya chama cha mapinduzi kuhakikisha kwamba tunawainua wananchi lakini mkakati wetu wa kufufua haya mazao ya kibiashara tunautekeleza kwa vitendo kwahiyo katika hili mimi nikushukuru  na niwaahidi tu Wizara ya kilimo itaendelea kutoa ushirikiano”

“ Lakini kipekee naomba nitoe shukrani zangu za dhati  kwa Mhe Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Wizara ya kilimo, nadhani tunaona sasa hakuna changamoto ya upatiukanaji wa mbolea kwani anatoa mbolea za ruzuku kwa kila mkulima , pia namshukuru Waziri wa kilimo Mhe. Hussein Bashe  kwa kuipambania wizara hii ya kilimo, pia shukrani zimuendee Mkuu wa  Mkoa wa Ruvua Kanal Laban Thomas kwa mapokezi yake mazuri na kutupa kibaria cha kufanya mkutano huu, pia nakushukuru Mkuu wa Wilaya ya Songea Kwa maandalizi ya Mkutano huu na Wadau wote wa Kilimo cha kahawa ambao nyinyi ndio mliotufanya sisi tuwepo mahali hapa.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Songea Mhe. Kapenjama Ndile amewataka wakulima kuacha kutegemea kilimo cha zao moja badala yake waongeze na kilimo cha kahawa kwani ni kilimo chenye tija hivyo kitawawezesha kuepukana na umasikini. Amesema

“ Tanzania inamazao mengi ya kimkakati ikiwemo kahawa, kwanini tunasema  ni zao la kimkakati kwasababu linaingizia fedha za kigeni taifa hili na kwa kufanya hivyo linapunguza umasikini kwa Watanzania, hivyo Wilaya ya Songea ni moja ya Wilaya iliyobahatika kuwa na hali ya hewa nzuri , udongo mzuri wenye rutuba  na maji ya kutosha ambayo yanachochea  uzalishaji wa zao la kahawa, hivyo ndugu zangu waku;lima tuamke sasa na kuchangamkia fursa hii na tunatakiwa tubadilike tuachane na kilimo cha msimu kwani  kahawa unaweza kupanda mwaka huu lakini ukawa unavuna mpaka unazeeka.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa zao la kahawa wilaya ya songea katika mkutano wa wadau wa kahawa songea  Frank Sungau amesema “ uzalishaji wa kahawa kwa msimu wa mwaka 2020/2021 wilaya ya songea  ilizalisha jumla ya Tani 1,888.43, mwaka 2021/2022 ilizalisha Tani 2,016.3 na mwaka 2022/2023 ilizalisha tani 3,040.89 ambapo mapato ya halmashauri yatokanayo na zao la kahawa ni , kwa 2020-2023 Halmashauri ya Wilaya ya Songea  ni 888,042,443.58, kwa Halmashauri ya Madaba ni  2,341,420.00 na Halmashauri ya Manispaa ya Songea ni 842,500.00”.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa