• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WAZIRI Dkt Ndumbaro afuta vibali vya uchomaji mkaa maeneo ya ushoroba

Tarehe ya Kuwekwa: April 24th, 2021

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Damas Ndumbaro amefuta vibali vyote vya uchomaji mkaa katika Vijiji vya Mbangamawe,Hangangadinda na Nderenyuma katika Kitongoji cha Kilimahewa maarufu kwa jina la“slow”katika Wilaya ya Madaba Mkoani Ruvuma kufuatia mgogoro wa wananchi na askari wa maliasili na wauhifadhi.

“Haiwezekani kuendelea kukata miti kuanzia leo vibali vyote vya mkaa vinakwisha”amesisitiza Dkt Ndumbaro.

Dkt Ndumbaro amefuta vibali hivyo kufuatia malalamiko na mgogoro unaodaiwa na wananchi wa Vijiji hivyo kuvamiwa na askari wa maliasili na wauhifadhi kuwataka waondoke kwenye makazi yao ambayo ni mapito ya asili ya wanyama pori kwa kuwachomea moto vibanda vyao na kuwapora mali zao mnamo Machi 5 na 6,2021.

Kufuatia malalamiko hayo Dkt Ndumbaro amefika katika Kijiji cha Mbangamwe na kufanya mkutano wa hadhara na wananchi pia kuhaidi kuunda tume itakayo washirikisha viongozi wa CCM ya kuchunguza madai ya malalamiko hayo kwa lengo la kubaini ukweli na uongo endapo kweli utabainika wahusika wote watachukuliwa hatua za kisheria pasipo kumwonea  mtu

Dkt Ndumbaro amesema wananchi hawatanyang’nywa maeneo yao wanayo yamiliki bali wataendelea kuyamiliki ,nje na makazi kwenye mashamba yao wataruhusiwa kufanya shughuli zinazo kwenda sambamba na  uhifadhi na utalii.

Dkt Ndumbaro amezitaja kazi ambazo wananchi wanatakiwa kufanya kwenye mashamba wanayo yamiliki kuwa ni upandaji wa miti ya kibiashara na ufugaji wa nyuki tu.

Dkt Ndumbaro amesema Wizara yake kupitia watalam wake wa Maliasili na Utalii watakwenda katika Vijiji hivyo kutoa elimu ya ufugaji nyuki na upandaji miti na kugawa mizinga kwa ajili ya kufugia nyuki bure kwenye vikundi vyote vilivyo sajiliwa.

Dkt Ndumalo amesema maeneo yote ya uhifadhi yanatakiwa kulindwa na kuhifadhiwa kwa manufaa ya Watanzania wote, hivyo wananchi waliouziwa maeneo kwenye hifadhi wafikirie kufanyakazi ya uhifadhi na sio vinginevyo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololeti Mgema amewatupia lawama viongozi wa Vijiji na Watendaji wake kwa kukiuka maagizo ya Serikali ya kuuza ardhi kiholela bila kufuata utaratibu na kuzalisha migogoro na malalamiko katika jamii.

Kwaupande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wa Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho ametoa wito kwa wananchi kuzingatia miongozo na maelekezo yanayotelewa na viongizi wa Serikali katika swala zima la kulinda na kutunza maliasili.

Amesema wananchi watakuwepo na ushoroba utakuwepo hivyo ni jukumu la viongozi kuwaelimisha wananchi kuhusu muhimu wa uwepo wa  maeneo ya uhifadhi na utalii katika makazi yao kitendo ambacho kitasaidia kuepusha purukushani baina yao na Serikali.

Historia inaonyesha kwamba katika kipindi cha miaka kati ya 1970 hadi 1986 katika maeneo  ya  Vijiji hivyo Wanyama pori walikuwa wakiishi na wakipita njia kuelekea upande wa pwani ya Msumbiji na kurejea Tanznia na vijiji hivyo vilikuwa bado havijasajiliwa.

Imeandaliwa na kuandikw na

Jacquelen Clavery

Afisa Habari Songea dc

24,04,2021




Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa