• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WAZEE WA WILAYA YA SONGEA, WAUNGANA NA WAZEE WENGINE DUNIANI KOTE KUADHIMISHA SIKU YA WAZEE DUNIANI

Tarehe ya Kuwekwa: October 1st, 2023

Kama ilivyo siku ya wanawake, siku ya watoto, siku ya baba, siku ya vijana siku ya mtoto wa kike, leo ni siku ya wazee duniani, hivyo wananchi wote duniani tunaungana ili kuadhimisha siku ya wazee kwa namna tofauti tofauti.

Siku ya wazee Duniani ilianzishwa na Umoja wa Mataifa mwaka 1990, kuwa siku ya kuhimiza na kupinga dhana na imani potofu kuhusu Wazee na uzee na kutambua umuhimu na mchango wao katika jamii

Dunia ilianza kutambua uwepo wa  Wazee mwaka 1959, hapa ndipo zilianza kutungwa sera mbalimbali  ila kutokana na kuimalika kwa huduma za afya, miundombinu mbali mbali ya kuhudumia wazee ilifanyika Sensa mwaka 1950 na kupata wazee million 200 kote dunian. Ambapo mpaka 2050, tunategemea kuwa na wazee million 700, na kwa Afrika kutakua na wazee million 350 mpaka ifikapo 2050.

 Kauli mbiu ya mwaka huu 2023 ni “UTHABITI WA WAZEE KWENYE DUNIA YENYE MABADILIKO” Siku hii Kitaifa itaadhimishwa Mkoani Geita October 06 2023, na kwa Wilaya ya Songea ilifanyika Kata ya Litisha kijiji cha Nakahuga September 29, 2023. Ambapo wao walikua na ujumbe usemao “UZEE NA KUZEEKA HAKUNA ATAYEKWEPA”

Katika maadhimisho hayo yaliyoratibiwa na Halmashauri ya wilaya ya Songea, mgeni Rasmi alikua Katibu Tawala wa Wilaya Mr. Mtela Mwampamba, aliyemuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Songea.  Ambapo pamoja na mambo mengine wazee walipewa Fursa ya kuonesha uwezo wao kwenye mambo mbalimbali  kama vile , Kucheza mpira wa miguu, kukimbikiza kuku, kuvuta kamba nk, pamoja na hayo wazee walionesha mazao mbalimbali wanayoyalima kwa ajili ya chakula lakini pia biashara.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa wilaya, Katibu Tawala wa Wilaya ya Songea  alisema “ niwaponge wazee wote kwa jinsi mlivyojitoa katika siku hii muhimu kwenu na kwetu, lakin kwa upekee niwaponge sana wakina babu na kina bibi walioshiriki katika michezo, kiukweli  mmetupa somo sisi vijana. Niwapongeze pia kwa jinsi mnavyoshiriki kwenye kilimo, nimeona mazao yenu Mahindi, Mpunga, Ndizi na Maharagwe ama kwa hakika ninyi ni wazee wa mfano na ndio maana Mhe Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameamua kuwekeza nguvu kubwa katika kuhakikisha vijiji vyote vinapata Mbolea ya Ruzuku  tena kwa Bei nafuu”


Aidha wazee pia walishauriwa kuwekeza nguvu yao kwenye kujishughulisha katika mambo mbalimbali ili kuepukana na magonjwa nyemelezi ambayo yamekua yakiwasumbua wazee wengi na kupelekea vifo vingi kwa wazee.

Dr. Geofrey Kihaule Mganga Mkuu wa Halmashauri ya  Wilaya ya Songea alisema “  tunapaswa kuangalia magonjwa yanayoambatana na uzee  kwa kuliangalia hilo ndio mana sisi kama serikali tumeamua kusimamia zoezi la upimaji wa afya kwa wazee wetu wote leo ili wajue matatizo yao na wapewe tiba. Lakini pia tunatambua wazee wanalishe duni ambayo hupelekea kupata magonjwa yanayotokana na changamoto ya lishe. Kutokufanya mazoezi kunachangia kinga za mwili kushuka”

Kwa upande wake Bi. Zawadi Nyoni aliyemuwakilisha Mkurugenzi mtendajiwa halmashauri, aliwashukuru wazee wote kwa kuitikia wito, na kujito kwa ajili ya siku hiyo muhimu, wadau mbalimbali waliochangia zoezi hilo kwenda kama lilivyopangwa na uongozi wa wilaya na serikali kuu kwa kusimamia vema jambo hili na kuona umuhimu wa wazee.


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa