• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WANANCHI WATAKIWA KUTUNZA VIFAA VYA UJENZI WA STENDI

Tarehe ya Kuwekwa: October 12th, 2023


Msimamizi wa asilimia kumi(10) ambazo ni nguvu za wananchi katika mradi wa ujenzi wa stendi ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea  Evagrini Kongwa amewaomba wananchi  kutoa ushirikiano hasa katika utunzaji wa vifaa vya ujenzi ili kukamilisha ujenzi huo kwa viwango sahihi.

Ameyasema hayo ikiwa utekelezwaji wa mradi huo umekwishaanza kwa kusafisha eneo ambapo pia kupitia nguvu za wananchi wamesogeza maji katika eneo la mradi ili ujenzi huo uanze maramoja. Amesema

“Shughuli ambazo tumefanya kwanza kabisa tumesafisha eneo ikiwa ni pamoja na kung’oa miti na kuweka eneo katika hali ya usawa (leveling)  kwaajili ya kuanza shughuli nyingine kama vile kuchimba msingi na hatua nyingine za ujenzi, pia shughuli nyingine ambayo tumefikia mpaka sasahivi tayari tumeshaingiza maji katika eneo la mradi  kama mchango wa nguvu za wananchi, baada ya hapo tunampango wa kujenga ghala  (store) la muda kwaajili ya kuhifadhia  vifaa, pia tutajenga choo cha muda kwaajili ya matumizi ya mafundi na wanafanyakazi wengine katika mradi huu, pia tunampango wa kuchimba mabwawa (malambo) kwaajili ya kuhifadhia maji ili kuwarahisishia mafundi watakapoanza ujenzi basi wasipate changamoto ya maji”.

“Kimsingi naomba nitoe rai kwa wananchi ambao wanauzunguka mradi huu kuweza kutunza mali au vitu tutakavyokuwa tunavileta hapa kwaajili ya shughiuli za ujenzi maana hizo ni mali zao kwani mali za Serikali ni mali za wananchi kwahiyo niombe kila mwananchi kuwa mlinzi kwa mwenzake katika kulinda mali hizo, pia natoa wito kwa wafanyakazi wa Halmashauri kuweza kutoa ushirikiano hata kwa ushauri tu kama kuna sehemu haijakaa sawa ni vema wakatoa ushauri ili kuboresha mradi huu na Halmashauri yetu ikapendeza kwa kupata stendi nzuri na yakisasa”

Aidha Mkurugenzi mtendaji wa Halimashauri ya Wilaya ya Songea Ndug Neema  M Maghembe, ameendelea kusisitiza kwa viongozi wote wanaohusika na kusimamia mradi huyo, kuhakikisha shughuli zinaenda kwa kufuata utaratibu na kujali muda waliopewa kwaajili ya kukamilisha ujenzi wa Stendi hiyo. 

“ Niendelee kuwasihi wasimamizi wa mradi huu, kusimamia vema ujenzi wa hii stendi, kwani uwepo wa stendi hii unafaida kubwa kwa wananchi wa Lundusi na Halmashauri kwa ujumla. Hivyo naamini watendaji wetu watajali muda tuliopewa wa kukamilisha ujenzi huo na kusimamia kwa weredi shughuli zote za ujenzi zinazoendelea. Tutaendelea kutoa ushirikiano kwa wataalam wetu wote kuhakikisha hawakwamishwi na chochote katika kutekeleza majukumu yao.

Mradi huu wa ujenzi wa stendi ulizinduliwa rasmi tarehe 16/08/2023 na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mhe.Jenista Joakim Mhagama na utaghalimu kiasi cha shilingi 434,657,802.68 ikiwa ni fedha kutoka Serikali Kuu kupitia TASAF na unatarajiwa kukamilika mwaka 2025


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa