• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WANANCHI wa Kijiji cha Peramiho (B) kujengewa soko la kisasa.

Tarehe ya Kuwekwa: November 30th, 2021

Serikali kupitia Mfuko wa kunusuru kaya masikini Nchini imetoa kiasi cha shilingi zaidi ya milioni 155 kwa ajili ya kujenga soko la kisasa katika Kijiji cha Peramiho (B) kilichopo Kata ya Peramiho Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma

Mratibu wa TASAF wa Halmashauri hiyo Hosana Ngunge amesema fedha hizo tayari zimeshaingizwa kwenye akaunti ya Kijiji kwa lengo la kuanza ujenzi  wa soko hilo ambalo utekelezaji wake utachukua muda wa miezi sita kufuatana na miongozo iliyotolewa na Serikali.

Ngunge ameitaja miundombinu ambayo itakayoanza kujengwa katika soko hilo kuwa ni choo matundu manne,vizimba na ghuba la taka.

Ngunge amesema TASAF kipindi cha pili awamu ya tatu imejikita zaidi katika kukuza uchumi wa kaya ambazo ni masikini sana kwa njia ya kutoa ruzuku ya fedha,ruzuku ya masharti,kuunda vikundi ambavyo vinajiwekea akiba na kukopeshana kwa riba nafuu kupitia fedha za ruzuku wanazozipata na ajira za muda mfupi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata hiyo Mhe Nikolaus Lutengano amewashukuru wananchi ambao wametoa maeneo yao kwahiari kwa nia ya kupisha ujenzi wa soko,na amehaidi kutoa ushirikiano wa kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa mradi hadi unakamilika na wananchi wake wanaanza kunufaika na huduma.

 Ameipongeza serikali na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa kusimamia na kufuatilia upatikanaji wa fedha hizo ambazo zinakwenda kutatua changamoto iliyokuwa ikiwakabili wananchi wa kijiji cha peramiho(B) cha kutokuwa na soko la kisasa.

Awali akizundua ujenzi wa soko hilo Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema ametoa rai kwa viongozi kusimamia mradi kwa umakini mkubwa na kuhakikisha mradi unatekelezwa vizuri na unatoa matunda chanya.

“Nataka soko lijengwe kwa miezi mitatu badala ya miezi sita ,“amesisitiza Mgema.

Mgema ametaka soko hilo lijengwe  kwa muda wa miezi mitatu kwa lengo la kuwasaidia baadhi ya wafanyabiashara kulinda na kutunza mitaji yao sanjari na kutoa fursa kwa wananchi kuanza kupata huduma za soko.

Ametoa wito kwa wananchi kuunga mkono jitihada za Serikali ambayo imekuwa ikitoa fedha nyingi katika utekeleza wa miradi mbalimbali ya maendeleo kama vile Afya,Maji,Barabara,Elimu na miundombinu mingine,kujitoa kwenye kusimamia na kujitolea nguvu zao wanapotakiwa katika kufanikisha lengo.

Ujenzi wa soko hilo la kisasa katika kijiji hicho unakwenda kutatua kero na changamoto za soko la uhakika na kuongeza mapato ya Halmashauri kupitia tozo na ushuru.

Imeandikwa na

Jacquelen Clavery

Songea DC    

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa