• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WALIMU Songea vijijini wakabidhiwa Vishikwambi

Tarehe ya Kuwekwa: January 13th, 2023

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe ameongoza zoezi la ugawaji vishikwambi kwa walimu wa shule za msingi na sekondari zilizopo Songea vijijini.

Zoezi hilo limefanyika tarehe 12 Januari katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri Lundusi-Peramiho ambapo vishikwambi 577 vimegawiwa kati ya 807 vilivyohitajika hivyo kuna upungufu wa vishikwambi 230 ili kukidhi mahitaji ya walimu wote.

Akizungumza katika zoezi hilo amewataka walimu kutunza zana hizo za kazi (vishikwambi) pamoja na maelekezo yote yaliyotolewa kutoka kwenye muongozo juu ya utunzaji na utumiaji ufuatwe.

“Tunakila sababu ya kuishukuru serikali yetu ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan pamoja na Mbunge wetu wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama kwa kuendelea kutuboreshea miundombinu katika sekta ya elimu”, amesema Ndugu Neema.

Akisoma muongozo wa vishikwambi Afisa Rasilimali watu na Utawala Ndugu Hashimu Lugome amesema vishikwambi ni mali ya serikali hivyo vitasimamiwa kwa mujibu wa sheria na kanuni ya manunuzi ya umma.

Ameongeza kuwa mwalimu aliyepokea kishikwambi endapo atastaafu, ataacha kazi, atafukuzwa au kufariki mali hiyo inapaswa irejeshwe serikalini.

‘’Vishikwambi hivyo vimeletwa kwaajili ya matumizi ya kujifunzia na kufundishia kwa walimu wa shule za msingi na sekondari na si kwa matumizi mengine hivyo mkishavipokea mkatekeleze kama masharti yalivyoelekezwa’’, amesisitiza Ndugu Lugome.

Akizungumza Afisa Elimu Msingi Bi Lucy Mbolu amewasisitiza walimu vishikwambi hivyo vitumike katika mambo ya msingi kama kutumiana maswali, kapakua vitu mbalimbali vya ufundishaji mtandaoni lengo ni kuongeza ufaulu katika shule za msingi na sekondari.

 Nae Afisa Elimu Sekondari Bi Bumi Kasege amewaasa walimu wazingatie usalama katika utunzaji wa vishikwambi hivyo pia amewaelekeza walimu waliopata vishikwambi hivyo waweze kushirikiana na wengine ambao hawajapata ili waendelee kuboresha ujifunzaji na ufundishaji shuleni.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa