• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WAKULIMA KUPIMIWA AFYA YA UDONGO BILA GHARAMA ZOZOTE.

Tarehe ya Kuwekwa: November 11th, 2023


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Ndg Neema M Maghembe amewasisitiza Maafisa kilimo wote ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuhakikisha wanapima afya ya udongo kwa wakulima bila kudai gharama zozote.

Ameyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya upimaji wa afya ya udongo yaliyofanyika 10/11/2023 katika ukumbi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea ambapo amewataka maafisa kilimo hao mpaka kufikia mwezi disemba wawe wamefikia malengo fulani katika kuwahudumia wakulima kupitia mafunzo hayo. Amesema 

" Wataalamu wenzangu natambua sana mchango wenu kwenye vijiji mpaka kwenye Kata zenu na inafahamika kwamba Kilimo ndio uti wa mgongo wa mapato ya Halmashauri yetu hivyo kupitia Elimu hii niwaombe ikawe chachu ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya Kilimo".

Lakini niwasisitize kitu kimoja mwongozo unatutaka tufanye shughuli hizi za upimaji wa afya ya udongo pasipo kumtoza mkukima gharama zozote nami nawaagiza nisisikie mkulima hajapimiwa udongo eti kwasababu hakuwa na fedha za kumuwezesha Afisa Kilimo kufanya hiyo shughuli hapo hatutaelewana, kwahiyo Mimi niwaombe tu ndugu zangu tukafanye kazi kadri ya miongozo tunayopewa". Alisema Ndg Neema M Maghembe Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea.

Nae Frank Sungau Afisa Kilimo wa makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea amesisitiza suala hilo na kutoa semina elekezi jinsi ya kuchukua sampuli ya udongo katika shamba la mkulima ambapo pia amewataka Maafisa kilimo hao kuhakikisha wanakwenda kwenye maeneo husika ya wakulima kuchukua taarifa zao. Amesema

"Pamoja na kufanya vipimo hivi bila gharama zozote basi niwaombe tuwe waaminifu katika kutoa taarifa za wakulima zilizo sahihi ikiwa ni pamoja na kufika shambani kwa mkulima na kuchukua sampuli ya udongo na kuja Kupima na sio umekaa kijiweni unajitungia taarifa za mkulima".


Baada ya mkulima kufanyiwa vipimo vya afya ya udongo wa shamba lake atapatiwa cheti cha uthibitisho wa kwamba shamba lake limefanyiwa vipimo vya afya ya udongo na cheti hicho pia atapatiwa bure bila gharama zozote na Kisha atashauriwa ni aina gani ya mbolea anatakiwa kutumia kutokana na vipimo vya udongo wa shamba lake.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa