• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WADAU SONGEA WAPEWA ELIMU YA UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Tarehe ya Kuwekwa: January 9th, 2026


Leo January 09 kumefanyika kikao cha kujengeana uwezo kuhusu utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, kikao ambacho kililenga kuwajengea uelewa wa kina wadau mbalimbali ili kuhakikisha mpango huo unatekelezwa kwa ufanisi, uwazi na kuwafikia wananchi wote bila ubaguzi wa aina yoyote.

Kikao hicho kiliwakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwemo wataalam wa afya kutoka vituo vya kutolea huduma za afya, watendaji wa kata na vijiji, pamoja na maafisa kilimo wa kata, ambao ni nguzo muhimu katika kufikisha elimu sahihi kwa wananchi ngazi ya jamii.

Akifungua kikao hicho, Katibu Tawala wa Wilaya ya Songea Ndug Mtela Mwampamba alisisitiza kuwa uelewa wa wananchi ni msingi muhimu wa mafanikio ya utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote. Alieleza kuwa pale wananchi wanapoelewa kwa kina malengo, faida na utaratibu wa mpango huo, huwa rahisi kuikubali, kujiunga nayo na kuitumia ipasavyo katika kupata huduma za afya

Ndug Mtela Mwampamba aliongeza kuwa bima ya afya ni ngao muhimu inayowaepusha wananchi na gharama kubwa za matibabu pindi wanapokumbwa na maradhi, na hivyo kuwawezesha kuendelea kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya jamii.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mhe George Ponera aliwataka wadau wote walioshiriki kikao hicho kwenda kuwa mabalozi wa elimu hiyo kwa wananchi katika maeneo yao ya kazi.

Alisisitiza kuwa Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa huduma bora za afya zinapatikana kwa wananchi wote bila kujali hali zao za kiuchumi au kijamii, na kwamba utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote ni sehemu ya mkakati mpana wa Serikali wa kuboresha sekta ya afya nchini.

Alieleza zaidi kuwa jukumu la wadau hao ni kuhakikisha taarifa sahihi, za kweli na zilizo rahisi kueleweka zinawafikia wananchi, kwa kutumia lugha nyepesi na mifano halisi ya maisha ya kila siku, ili kuondoa hofu, dhana potofu na taarifa zisizo sahihi ambazo zimekuwa zikikwamisha mwitikio wa wananchi kujiunga na mpango wa bima ya Afya.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • PPRA KANDA YA KUSINI YATOA MAFUNZO YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA KWA WATUMISHI SONGEA DC

    January 13, 2026
  • MAAGIZO 10 YA NAIBU WAZIRI KWAGILA; WATAALAM WATAKIWA KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA MIRADI

    January 11, 2026
  • WADAU SONGEA WAPEWA ELIMU YA UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 09, 2026
  • MWAMPAMBA AIPONGEZA SONGEA DC NA KUSISITIZA MIKOPO YA 10% IENDELEE KUTOLEWA.

    January 08, 2026
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa