• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MAAGIZO 10 YA NAIBU WAZIRI KWAGILA; WATAALAM WATAKIWA KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA MIRADI

Tarehe ya Kuwekwa: January 11th, 2026


Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mhe. Ruben Kwagila (MB), ametoa maelekezo 10 mahususi kwa wataalam na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, akisisitiza umuhimu wa nidhamu ya fedha, usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo na matumizi sahihi ya mifumo ya Serikali.

Mhe. Kwagila alitoa maelekezo hayo Januari 10, 2026, wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Shule ya Sekondari Amali Lundusi na Shule ya Sekondari Jenista Mhagama, sambamba na kupokea taarifa ya mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mh. Prof. Riziki Shemdoe, Naibu Waziri alisema maelekezo hayo ni mwongozo wa jumla wa Wizara unaopaswa kuzingatiwa na Mamlaka zote za Serikali za Mitaa.

Kwanza, alisisitiza nidhamu katika makusanyo ya mapato ya ndani na matumizi ya fedha za umma, akisema “tukusanye kwa nidhamu na tutumie kwa nidhamu, ndipo tutakapopata matokeo chanya”. Aliwataka watumishi wote kuzingatia matumizi sahihi ya fedha za Serikali.

Pili, aliagiza miradi yote isimamiwe kikamilifu hadi kukamilika, akisisitiza kuwa bajeti zielekezwe kwanza katika kukamilisha miradi iliyopo kabla ya kuanzisha mipya. Alifafanua kuwa TAMISEMI imeigawa nchi katika kanda kwa kuzingatia gharama za ujenzi na malighafi, hivyo upangaji wa bajeti uzingatie uhalisia huo.

Tatu, aliagiza hoja zote za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) zijibiwe na maelekezo pamoja na ushauri wa Kamati zote za Bunge yatekelezwe kikamilifu ili hoja ziondoke kwenye vitabu vya Serikali.

Nne, alisisitiza matumizi ya mifumo ya Serikali akieleza kuwa TAMISEMI ni daraja la utekelezaji wa sera zote za Wizara. Alikataza ukusanyaji wa mapato nje ya mfumo wa TAUSI, matumizi ya fedha kupitia MUSE, na manunuzi kufanyika kupitia NEST, akisisitiza matumizi ya mifumo hiyo bila kukoma.

Tano, aliagiza fedha za ndani zipelekwe kwenye miradi kwa kuzingatia mipango na bajeti, sambamba na kulipa madeni ya wazabuni kwa wakati ili kuwawezesha kuendelea kutoa huduma bila kuyumbishwa kiuchumi.

Sita, alielekeza fedha za mikopo zitolewe kulingana na makusanyo halisi, mikopo itolewe kwa ukamilifu na isimamiwe kikamilifu ili fedha za Serikali zirejeshwe na wanufaika wengine waweze kunufaika.

Saba, aliagiza maeneo yote ya mali za Serikali ikiwemo ofisi za Halmashauri, shule, hospitali, vituo vya afya na zahanati yapimwe na kupatiwa hati miliki. Alisisitiza fedha zitengwe kwenye bajeti ili kuepuka migogoro ya ardhi isiyo ya lazima.

Nane, aliwataka watumishi kufanya kazi kwa bidii kila mmoja kwa ngazi yake, kuanzia vitongoji, vijiji, kata, tarafa hadi Halmashauri, akisisitiza kuwa kero za wananchi zisikilizwe na kutatuliwa kwa wakati.

Tisa, alisisitiza umuhimu wa ukaguzi wa mara kwa mara (routine inspection), akiwataka wataalam kuyafahamu majukumu yao, kuijua miradi na kuitembelea mara kwa mara ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji.

Kumi, aliwataka watumishi kuzingatia Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2009, maadili ya utumishi na kanuni za mienendo (Code of Conduct), akisisitiza kuwa ni wajibu wa Maafisa Utumishi kusimamia sheria na maadili hayo.

Naibu Waziri alihitimisha kwa kuwataka wataalam na viongozi wote wa Serikali za Mitaa kuyatekeleza maelekezo hayo kwa vitendo ili kuhakikisha miradi ya maendeleo inawanufaisha wananchi na kuleta tija iliyokusudiwa.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • PPRA KANDA YA KUSINI YATOA MAFUNZO YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA KWA WATUMISHI SONGEA DC

    January 13, 2026
  • MAAGIZO 10 YA NAIBU WAZIRI KWAGILA; WATAALAM WATAKIWA KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA MIRADI

    January 11, 2026
  • WADAU SONGEA WAPEWA ELIMU YA UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 09, 2026
  • MWAMPAMBA AIPONGEZA SONGEA DC NA KUSISITIZA MIKOPO YA 10% IENDELEE KUTOLEWA.

    January 08, 2026
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa