• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

PPRA KANDA YA KUSINI YATOA MAFUNZO YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA KWA WATUMISHI SONGEA DC

Tarehe ya Kuwekwa: January 13th, 2026


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bwa. Exavery Luyagaza, leo Januari 13, 2026, amefungua mafunzo ya Sheria ya Ununuzi wa Umma kwa watumishi wa Halmashauri hiyo, yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) Kanda ya Kusini, yakilenga kuongeza ufanisi na uwajibikaji katika ununuzi wa serikali.

Akizungumza wakati anafungua mafunzo hayo, Bwa. Exavery aliishukuru PPRA kwa kuandaa mafunzo hayo muhimu, akieleza kuwa yamekuja katika kipindi muafaka ambapo Halmashauri inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayohitaji usimamizi makini wa michakato ya ununuzi.

“Mafunzo haya yatatuwezesha kuongeza uelewa wetu kuhusu Sheria mpya ya Ununuzi wa Umma na yatajibu changamoto nyingi ambazo tumekuwa tukizipata katika utekelezaji wa majukumu yetu. Kupitia mafunzo haya, watumishi watajifunza kwa kina wajibu wao katika kuhakikisha ununuzi unafanyika kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa,” alisema Bwa. Exavery.

Aliongeza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Songea imejipanga kuyatumia maarifa yatakayopatikana ili kuboresha mifumo ya ndani ya ununuzi, kuimarisha usimamizi wa zabuni na mikataba, pamoja na kuongeza uwajibikaji kwa watumishi wote wanaohusika na shughuli za ununuzi.

Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo Bwa. Michael Ibrahim mtaalamu wa PPRA Kanda ya Kusini, alibainisha kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati endelevu wa mamlaka hiyo wa kuhakikisha taasisi zote za umma zinaelewa kikamilifu Sheria ya Ununuzi wa Umma na kuitekeleza kwa ufanisi, sambamba na kuimarisha misingi ya utawala bora katika ngazi zote za Serikali.

Mafunzo hayo yalifanyika katika mazingira ya kujifunza yaliyoruhusu majadiliano ya wazi, maswali na majibu, pamoja na uwasilishaji wa mada mbalimbali zilizojikita katika tafsiri ya Sheria mpya ya Ununuzi wa Umma, mabadiliko yaliyofanyika ikilinganishwa na sheria ya awali, pamoja na wajibu wa kila mdau katika kuhakikisha ununuzi unafanyika kwa kuzingatia misingi ya uwazi, ushindani wa haki na thamani halisi ya fedha.

Katika mafunzo hayo, wataalamu wa PPRA walieleza kuwa lengo kuu la mafunzo ni kujenga

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • PPRA KANDA YA KUSINI YATOA MAFUNZO YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA KWA WATUMISHI SONGEA DC

    January 13, 2026
  • MAAGIZO 10 YA NAIBU WAZIRI KWAGILA; WATAALAM WATAKIWA KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA MIRADI

    January 11, 2026
  • WADAU SONGEA WAPEWA ELIMU YA UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 09, 2026
  • MWAMPAMBA AIPONGEZA SONGEA DC NA KUSISITIZA MIKOPO YA 10% IENDELEE KUTOLEWA.

    January 08, 2026
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa