• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

VIKUNDI 28 VAPATIWA MIKOPO YA TSH MILIONI 249 NA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

Tarehe ya Kuwekwa: July 3rd, 2025


Halmashauri ya Wilaya ya Songea kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii imetoa mikopo yenye jumla ya Tsh 249,014,000 kwa vikundi 28 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, fedha ambazo zinatokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Akizungumza wakati wa kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya mikopo hiyo, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Songea, Bi Zawadi Nyoni, alieleza kuwa Halmashauri ilipokea jumla ya maombi kutoka kwa vikundi 62, lakini ni vikundi 28 pekee ndivyo vilivyokidhi vigezo na kupatiwa mikopo hiyo. Alibainisha kuwa kati ya fedha hizo, Tsh milioni 116.5  zilitolewa kwa vikundi 15 vya wanawake, Tsh milioni 116.5 kwa vikundi 7 vya vijana, na Tsh 14,014,000 kwa vikundi 6 vya watu wenye ulemavu.

Bi Zawadi alieleza kuwa fedha hizo tayari zimeingizwa kwenye akaunti za vikundi husika na kusisitiza kuwa ni wajibu wa wanufaika kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kujiwezesha kuleta maendeleo ya kweli kwa jamii na kurahisisha urejeshaji wake kwa wakati.

Katika mafunzo hayo, wanachama wa vikundi walielimishwa kuhusu umuhimu wa kuweka kumbukumbu sahihi za matumizi ya fedha, kubuni miradi yenye tija, na kuwa na mpango wa marejesho endelevu ili kuhakikisha mzunguko wa mikopo hiyo unawanufaisha wananchi wengi zaidi katika siku zijazo.


Idara ya Maendeleo ya Jamii imejipanga kuendelea kutoa elimu kwa vikundi mbalimbali kabla na baada ya utoaji wa mikopo ili kuongeza ufanisi wa matumizi ya fedha hizo na kuboresha hali ya maisha ya wananchi wa Wilaya ya Songea, hasa makundi maalum yanayolengwa na mikopo hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI 28 VAPATIWA MIKOPO YA TSH MILIONI 249 NA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    July 03, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

    July 01, 2025
  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa