• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

UONGOZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea wamefanya utambulisho wa mradi Matomondo

Tarehe ya Kuwekwa: February 27th, 2023



Halmashauri ya Wilaya ya Songea imepokea fedha kiasi Cha shilingi Milioni 198, 700,650 kutoka Serikali kuu Kwaajili ya ujenzi wa ghala na soko katika Kijiji cha Matomondo.

Hayo yamethibitishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshimiwa Menas komba katika mkutano wa hadhara wa kutambulisha mradi Kwa wananchi.

Aidha, katika mkutano huo ulioambatana na zoezi la utambulisho wa kamati ya ujenzi ambayo itasimamia utekelezaji wa mradi.

Akizungumza Mheshimiwa Komba amezitaka kamati za ujenzi kuwa na ushirikiano baina yao ili mradi uweze kukamilika Kwa wakati na viwango vinavyokubaliwa na Serikali.

" Napenda kuchukua nafasi hii kuwasisitiza kamati zote zinazohusika na ujenzi ikiwemo kamati ya manunuzi na mapokezi  hakikisheni mnanunua vifaa vyenye ubora ili hili soko liweze kudumu na litumike Kwa vizazi na vizazi", amesisitiza Mheshimiwa Komba.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema maghembe ametoa shukrani Kwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama Kwa kuleta fedha hizo Kwaajili ya ujenzi wa soko ambalo linaenda kusaidia wakulima kuuza mazao na kuinua uchumi.

Ndugu Neema amesema mradi ni wa wananchi wote hivyo Kila mmoja ana wajibu wa kuhakikisha mradi unaisha Kwa muda uliopangwa.

"Tumekuja kufafanua ili Kila mmoja katika Kijiji awe na uelewa na huu mradi hivyo nawasisitiza Kila mtu aguswe afanye wajibu wake panapotakiwa nguvu za wananchi naomba mjitoe ili huu mradi ukamilike mapema", amesisitiza Ndugu Neema.

Pia amewahasa kamati zinazosimamia mradi pamoja  na watumishi wanasimamia mradi kuwa waadilifu na wenye weledi mkubwa ili kuhakikisha mradi unajengwa kwa ubora na viwango vinavyotakiwa na kwa thamani halisi ya fedha

Vilevile amesisitiza kuwa hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayebainika kuweka maslahi binafsi mbele na kwenda kinyume na taratibu za manunuzi ya vifaa vya ujenzi wa mradi na usimamizi wa mradi kwa ujumla.

Akizungumza Diwani wa Kata ya Mbinga Mhalule Mheshimiwa Nasri Nyoni ameushukuru uongozi wa Halmashauri Kwa kuja kutambulisha mradi na kujenga uelewa Kwa wananchi hivyo ameahidi kushirikiana vyema na viongozi wa Kata na Kijiji pamoja na wananchi ili kuhakikisha mradi huu unakamilika Kwa viwango.

Nae Afisa Kilimo Wilaya Bi Hellen Shemzigwa amesema Serikali imeleta fedha hizo Kwa dhamira ya kusaidia mkulima ili asisumbuke na mazao hivyo amewataka wananchi wa Matomondo kuupenda na kuheshimu mradi huu Kwa maslahi yao.

Wakizungumza wananchi wa Kijiji cha Matomondo wamemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Kwaajili ya kuleta fedha za ujenzi wa soko ambalo linaenda kutatua changamoto katika uuzaji wa mazao.


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa