• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Ujenzi wa Hosteli

Tarehe ya Kuwekwa: July 10th, 2018

UJENZI WA HOSTELI

Halmashauri  ya wilaya  ya Songea, mkoani  Ruvuma  imekamilisha  ujenzi  wa hosteli katika  shule ya  Sekondari Barabarani kwa asilimia 85 kupitia  mpango  wa lipa  kutokana na matokeo(EP4R)

 Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Halmashauri  ya Wilaya ya  Songea Bw Simoni  Bulenganija  amesema  mpango    wa  EP4R utasaidia  wanafunzi kutojiingiza katika  vishawishi ambavyo  vitakavyopelekea   kupata  mimba  na  utoro na kukatisha  masomo. 

 Amesema  Serikali  kupitia  Halmashauri imejipanga  kuhakikisha  mazingira ya kujifunzia  na  kufundishia yanaboreshwa kwa kujenga  hosteli kwa ajili ya  wanafunzi  wa kike  na wavulana  wanaoishi  mbali   na mazingira shule kazi  ambayo  inaendelea  kwa  sasa  katika  Halmashauri  hiyo.

 Amesema hosteli hiyo itakapokamilika itapunguza adha kubwa kwa wanafunzi ya kupanga vyumba kwa ajili ya   kulala. Aidha hosteli hiyo inauwezo wa kutoa huduma ya malazi kwa wanafunzi 170   kati yao wasichana 85 na wavulana 85. 

Bw Bulenganija  amesema  kwa sasa  ujenzi huo  umekamilika  kwa  asilimia  85  huku  akiwashukuru  wananchi  wa  kijiji  hicho  cha  Muhukuru Barabarani  kwa kuonyesha  ushirikiano   katika kipindi   cha ujenzi  wa hosteli kwa ulinzi shirikishi.

 Alisema  asilimia  15  zilizobaki   kwa ajili ya kukamilisha  ujenzi  huo  pamoja  na kazi za   kupachika  milango, madirisha   na kupaka  rangi , kazi hiyo  itakapo kamilika  hosteli  hiyo  itaanza  kutoa huduma  mara  moja  kwa  wanafunzi ambao  kwa sasa  wanakaa  nje ya mazingira  ya  shule  kwa  kupanga   nyumba .

 Naye  diwani  wa  kata  ya  Muhukuru katika  Halmashauri  ya Songea Manufred  Mzuyu  alipohojiwa  na  mwandishi  wa habari hizi  alisema  mradi  huo  ulitakiwa  kukamilika  mwezi    Machi  30  mwaka huu lakini  anashangaa  hadi  hivi  sasa mradi huo   haujakamilika  na  wanafunzi  wanaendelea  kuishi  kwa  kupanga  nyumba  za  wenyeji  kitu  ambacho  alidai  ni hatari  kwa  wasichana  kutokana  na vishawishi  vya kupata  mimba  na  utoro.

Kwa upande  wake  Mhandisi wa halmashauri   ya wilaya  ya  Songea Bw Frank  Hosea  alisema  ujenzi  huo  wa  hosteli  umechelewa  kukamilika  kwa wakati  kutokana  na jiografia  ya  hamlashauri  hiyo  katika kipindi  cha masika  miundo  mbinu  hasa  barabara  zilikuwa  hazipitiki  na kushindwa  kusafirisha  vifaa  vya  viwandani  kufika  katika  eneo  la mradi.Mradi huo umegharimu jumla ya shilingi milioni 150 hadi kukamilika kwake.

JACQUELEN CLAVERY-TEHEMA     

 

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa