• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SONGEA DC imepokea Milioni 250 kutoka Serikali kuu.

Tarehe ya Kuwekwa: September 15th, 2022

HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea imepokea shilingi Milioni 250 kutoka Serikali Kuu kuanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa shule ya msingi Lizaboni ambayo inajengwa katika kijiji cha Muhukuru Barabarani.

Hayo yamethibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe ambae amewakilishwa na Afisa Elimu Sothery Nchimbi wakati wa kikao na wananchi wa kijiji cha muhukuru Barabarani.

Hata hivyo amesema lengo la kikao hiko ni kutambulisha mradi kwa wananchi, kuunda kamati ambazo zitasimamia zoezi zima la utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa shule pamoja na kupima maeneo.

‘’Nawaomba kamati zote ambazo zimechaguliwa tuhamasike, tujihamasishe na tuwahamasishe wananchi wengine pale ambapo inahitaji kujitoa hasa katika kulinda vifaa tujitoe kwelikweli ili ujenzi wetu uweze kwenda vizuri na kukamilika kwa wakati’’, amesisitiza Afisa Elimu Nchimbi.

Ametoa rai kwa wananchi wawajibike katika ujenzi huu pale ambapo zinahitajika nguvu za wananchi basi waweze kujitoa na kujituma ili kuhakikisha mradi unakwenda vizuri.

Kwaupande wake mwenyekiti wa Kitongoji Ndugu Semblini Komba amewashukuru wajumbe kwa elimu waliyoitoa na ameahidi yote yaliyosemwa watayafuata na kuwa kipaumbele katika kuwaelekeza wengine.

Wakizungumza wananchi wa kijiji cha Mhukuru barabarani wameishukuru Serikali ya awamu ya sita ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Mbuge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama.

Pia wamemshukuru Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mheshimiwa Menace Komba, Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Neema Maghembe, Diwani wa kata ya Muhukuru Barabarani Mheshimiwa Manfred Mzuyu pamoja na Watendaji wote kwa kuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Imeandaliwa na Bahati Nyoni,

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

Septemba 15, 2022.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa