• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SILINDE kuendelea kusimamia ujenzi wa miundombinu ya elimu

Tarehe ya Kuwekwa: December 18th, 2021

Naibu Waziri wa Elimu TAMISEM David Silinde amehaidi kuendelea kusimamia ujenzi wa miundombinu ya elimu kwalengo la kuboresha mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia.

Silinde ametoa ahadi hiyo alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa kupitia mradi wa Mpango wa maendeleo wa Ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19 katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea hivi  karibuni

Silinde amesema ataendelea kusimamia na kuhakikisha miundombinu ya kutolea elimu inajengwa na mazingira ya kujifunzia na kufundishia ya na kuwa bora na mazuri kwa walimu na wanafunzi.

“Mimi ni mkali lakini kwa miradi hii napongeza”,amesisitiza Silinde

Silinde amewapongeza viongozi na wadau walioshiriki kutekeleza ujenzi wa vyumba hivyo kwa kuzingatia maagizo na maelekelezo yaliyotolewa na serikali  kwakwenda na muda wa ukamilishaji wa miradi hiyo.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi. Neema Maghembe amesema jumla ya vyumba vya madarasa 65 vimejengwa na kukamilika kati ya hivyo vyumba 46 vimejengwa kwenye shule za sekondari zote za Serikali ambazo ni 16,madarasa 19 yamejengwa kwenye vituo shikizi vya shule za msingi tano.

Ameongeza kwakusema wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2022 hakuna atakayebaki nyumbani kwakigezo cha kukosa vyumba vya madarasa wote wataanza masomo kulingana na taratibu,sheria, kanuni na miongozo ya nchi.

Halmashauri ya Wilaya ya Songea ilipata mgao wa fedha toka Serikalini jumla ya shilingi Bilioni 1.3 kwaajili ya kujenga vyumba 65 vya madarasa na kila darasa limegharimu shilingi miloni 20 pamoja na madawati yake kwa shule shikizi za msingi ,meza na viti kwa upande wa sekondari.

Imeandaliwa na kuandikwa na

Jacquelen Clavery.

 


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa