• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

RUWASA kutumia Milioni 848 kumaliza kero ya maji Kijiji cha Parangu

Tarehe ya Kuwekwa: April 3rd, 2022

MKUU wa Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma Pololet Mgema amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi wa Mama Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa kiasi cha shilingi milioni 848 kujenga mradi wa maji katika Kijiji cha Parangu kilichopo Kata ya Parangu,

Mgema  ameyasema hayo wakati akikabidhi miundo mbinu ya ujenzi wa miradi ya maji katika kijiji hicho kwenye hafla fupi iliyofanyika hivi karibuni katika Shule ya Sekondari ya Jenista Mhagama iliyojengwa katika kijiji hicho.

“Napenda nitumie fursa hii kumpongeza Rais wetu Mhe.Samia Suluhu  Hassani kwakutupa fedha nyingi katika Wilaya yetu ya Songea katika sekta zote za ujenzi wa miradi,”amesema Mgema.

Kwaupande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Menas Komba amemshukuru  Mbunge wa Jimbo hilo Mhe Jenista Mhagama kwa ufuatiliaji wa fedha kutoka Serikali kuu ambazo zinatekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kushirikiana na  viongozi na wadau wengine wa maendeleo 

  .

Mhe.Komba  amesema kuwa Serikali imekuwa ikifanya kazi kubwa katika kuwaletea wananchi maendeleo kusudiwa kulingana na ilani ya Ccm ya mwaka 2020-2025 na kwamba kazi kubwa hivyo  wao kama viongozi jukumu lao ni kusimamia fedha zinazotolewa na Serikali zinatekeleza ujenzi wa shughuli za miradi kama ilivyokusudiwa.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bernadetha Mapunda ameishukuru Serikali kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Mijini na Vijijini(RUWASA ) Songea kwa kuwajengea mradi huo wa maji ambao utawasaidia kuokoa muda wa kufuata maji umbali mrefu kwenye visima vya asili, pia utawaondolea maradhi yatokanayo na maji yasiyosafi na salama

Mapunda amesema kupitia mkutano wa hadhara walioketi wameadhimia kumtia hatiani mtu yoyote atakayebainika anaharibu vyanzo vya maji na atakayekaidi kuchangia gharama za huduma za maji ambazo ni shilingi 2000/= kiwango ambacho wamekubaliana

Aidha Meneja wa Ruwasa wilaya ya Songea Mhandisi Mathias  Charles amesema mradi huo wa kijiji cha Parangu utajengwa umbali wa kilometa 19.55 ambapo kukamilika kwake utahudumia wananchi wapatao zaidi ya 3,000 na kwamba mradi huo umeanza kujengwa na utakamilika ifikapo mwezi juni 2022

Mhandisi Charles amewasisitiza wananchi kuendelea kutoa ushirikiano wa kupanda miti kwenye vyanzo vya maji, kuacha kufanya shughuli za kibinadamu kwenye maeneo ya vyanzo vya maji kwani shughuli hizo zinaathiri vyanzo hivyo

Ameitaja miradi mingine ambayo inatekelezwa na Ruwasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuwa ni mradi wa maji Mtiririko wa Matimira na Mpitimbi B kwa jumla ya gharama ya bilioni 1.6

Imeandikwa na

Jacquelen Clavery

Afisa Habari

Songea dc

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa