• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MKUU WA WILAYA YA SONGEA AWAPONGEZA WATENDAJI WA HALMASHAURI KWA KUSIMAMIA VIZURI UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA LISHE BORA

Tarehe ya Kuwekwa: June 11th, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe.  Kapenjama Ndile, amewapongeza Wataalam na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea pamoja kwa kazi nzuri ya kusimamia na kuboresha vizuri utekelezaji wa shughuli za lishe katika maeneo yao.

Akizungumza katika kikao cha lishe Cha robo ya tatu 2024/2025 kilichofanyika leo katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mheshimiwa Ndile alisema:“Halmashauri hii inafanya vizuri sana katika kuimarisha lishe bora kwa watoto. Pongezi nyingi kwenu kwa kazi nzuri mnayoifanya kwa ustawi wa jamii yetu.”

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya aliwataka watendaji kuongeza juhudi zaidi katika kata ambazo bado zina viwango vya chini vya lishe “Ni muhimu kuongeza nguvu na ubunifu katika kata ambazo hali ya lishe bado haijaridhisha, ili kuhakikisha kila mtoto anapata lishe bora bila kujali eneo analotoka,” alisisitiza.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi Elizabeth Gumbo, alitoa pongezi kwa watendaji wa kata kwa usimamizi wao mzuri wa masuala ya lishe.

“Napenda kuwapongeza sana kwa jitihada zenu. Kupitia kazi yenu, Halmashauri yetu imeendelea kuwa katika nafasi nzuri katika hali ya lishe,” alisema Bi. Gumbo.

Katika kikao hicho, Afisa Lishe wa Halmashauri, Bi Joyce Sipira, aliwasilisha taarifa ya hali ya lishe kwa kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 ambapo pamoja na mambo mengine alielezea mafanikio yaliyopatikana ambayo ni pamoja na kuwajengea uwezo watoa huduma wa vituo vya afya kuhusu utekelezaji wa huduma za lishe, hatua ambayo inalenga kuboresha huduma kwa watoto na akina mama.

Aidha, Bi Sipira alieleza kuwa wasindikaji wa unga wa mahindi wamepatiwa vifaa maalum vya kuongeza virutubishi (vinyunyizi) na mashine zao kufungiwa mifumo ya kuongeza virutubishi kwenye unga, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kupambana na upungufu wa vitamini na madini.

Kikao hicho kimeonyesha dhamira ya pamoja ya Halmashauri, viongozi na wadau katika kuhakikisha hali ya lishe inazidi kuimarika hasa kwa watoto, ili kujenga kizazi chenye afya bora na chenye mchango chanya kwa taifa.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • WASIRA ATIA NENO UKAMILISHAJI WA MIRADI SONGEA DC, AMPONGEZA DKT. SAMIA

    June 12, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA SONGEA AWAPONGEZA WATENDAJI WA HALMASHAURI KWA KUSIMAMIA VIZURI UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA LISHE BORA

    June 11, 2025
  • MATUMIZI YA LISHE ILIYO BORA YASISITIZWA MASHULENI

    June 10, 2025
  • KITUO CHA AFYA MATIMILA CHAKABIDHIWA GALI LA WAGONJWA.

    June 06, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa