• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MKUU wa shule afikishwa Mahakamani kwa rushwa

Tarehe ya Kuwekwa: May 23rd, 2019

TAASISI ya Kuzuia na  Kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoani Ruvuma imemfikisha katika Mahakama ya Wilaya ya Namtumbo Mkuu wa shule ya sekondari Nanungu Mohamed Shafii Ngonyani kwa makosa ya rushwa.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake Mahenge mjini Songea,Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Owen Jasson  amesema Mkuu huyu wa shule na aliyekuwa Msimamizi Mkuu wa Mitihani ya kidato cha sita mwaka huu 2019 Vitus Johnson Matembo wanakabiliwa na makosa ya rushwa kinyume na kifungu cha 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka 2007.

Jasson amebainisha kuwa Mei 7,2019 Ofisi ya TAKUKURU ilipokea taarifa kutoka chanzo cha siri ikimtuhumu Mkuu wa shule hiyo kwa makosa ya kuwashawishi wasimamizi wa mitihani ya kidato cha sita 2019 katika shule hiyo kwa kutaka kuwapatia fedha za hongo kiasi cha shilingi 100,000 ili walegeze masharti ya usimamizi wa mitihani kwa wanafunzi wanaofanya mitihani katika shule hiyo.

“Baada ya kupokea taarifa hiyo,uchunguzi ulifanyika ambapo ilithibitika kwamba ni kweli washitakiwa hao wawili walishirikiana kufanya kitendo cha rushwa ambapo Ndugu Vitus Johnson Matembo alishawishika na kupokea fedha hizo ili akagawane na wenzake’’,alisisitiza Jasson.

Hata hivyo Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma amesema wenzake walikataa kushawishika na kwamba watuhumiwa  hao wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya  ya Namtumbo na kusomewa mashitaka yao.

Jasson kupitia kwa wanahabari amewapongeza wasimamizi wote wa mitihani ya kidato cha sita waliokataa vishawishi hivyo vya rushwa na kusimamia mitihani hiyo kwa uadilifu kama inavyotakiwa.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa