• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

Tarehe ya Kuwekwa: October 21st, 2025


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi. Elizabeth Mathias Gumbo, ametoa wito kwa wananchi na watumishi wote wa Halmashauri hiyo kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi la kupiga kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Akizungumza ofisini kwake, Gumbo amesema kuwa maandalizi ya uchaguzi huo yanaendelea vizuri katika maeneo yote ya Wilaya ya Songea, huku akisisitiza umuhimu wa wananchi kutumia haki yao ya kikatiba kushiriki katika uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani

Ameeleza kuwa vituo vyote vya kupigia kura vitafunguliwa kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni, na hivyo amewataka watumishi wa umma pamoja na wananchi wote kuhakikisha wanapanga muda wao mapema ili waweze kushiriki bila kisingizio. “Ni jukumu la kila mmoja wetu kuhakikisha tunatimiza wajibu huu wa kitaifa, kwani kura yako ndio sauti yako na ndiyo chachu ya mabadiliko tunayoyataka,” alisema.

Aidha, Mkurugenzi huyo amewahimiza wananchi kutambua kuwa kushiriki kupiga kura ni njia pekee ya kuchagua viongozi bora watakaosimamia maendeleo yao, Ameongeza kuwa mara nyingi wananchi hulalamika kuhusu viongozi wasio na ufanisi, lakini changamoto kubwa imekuwa ni watu wengi kutojitokeza kupiga kura licha ya kuwa ni haki yao ya msingi.

“Wananchi wengi wamekuwa wakisema wanahitaji viongozi bora, lakini hawajitokezi siku ya kupiga kura haki hii ni ya msingi na ni wajibu kwa kila mmoja kuhakikisha anaitumia kwa busara ili kuchagua viongozi watakaoharakisha maendeleo katika maeneo yetu,” alisisitiza.

Katika maandalizi ya kuelekea siku ya uchaguzi wananchi wanapaswa kutembelea vituo walivyojiandikisha ili kuthibitisha majina yao kwenye orodha ya wapiga kura, na pia kujionea karatasi ya mfano wa kupigia kura ambayo itaonesha namna sahihi ya kuweka alama ya kura. Hatua hiyo ni muhimu kwani itawasaidia wananchi kuepuka makosa yatakayoweza kusababisha kura zao kuharibika.

kwa mujibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi siku ya uchaguzi wanachi wanapaswa kufika vituoni wakiwa na kadi ya mpiga kura au kitambulisho cha taifa (NIDA) au, leseni ya udereva, au kitambulisho kingine chenye majina yanayofanana na yale waliyojiandikishia, kama uthibitisho wa utambulisho wao.

Katika hatua nyingine Halmashauri ya Wilaya ya Songea imekuwa mstari wa mbele katika kuhimiza uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi katika shughuli za maendeleo, na uchaguzi ni mwendelezo wa juhudi hizo.

“Kura yako ni haki yako, Jitokeze kupiga kura" Kwa ujumla, kauli mbiu hii inahamasisha uzalendo, uwajibikaji na ushiriki wa wananchi katika mchakato wa demokrasia kwa njia ya amani. Inalenga kuondoa visingizio vya kutojitokeza kupiga kura na kuhimiza kila raia kuelewa kuwa maendeleo ya taifa yanaanza na kura yake.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

    October 23, 2025
  • WATAHINIWA 5157 WA DARASA LA NNE SONGEA DC, WAANZA MITIHANI YAO LEO

    October 22, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 21, 2025
  • SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

    October 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa