• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

Tarehe ya Kuwekwa: October 18th, 2025


Katika kuendelea kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi, Serikali Kuu kupitia Wizara ya Afya imetoa zaidi ya shilingi milioni 891 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya viwili ambavyo vitasaidia zaidi ya wananchi 23,800 walipo katika Kata ya Peramiho na Mpandangindo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma.

Fedha hizo zinajumuisha kiasi cha shilingi milioni 641,627.778 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Peramiho, na shilingi milioni 250,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Mpandangindo.

Akizungumza baada ya mapokezi ya fedha hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi. Elizabeth Gumbo, alisema fedha hizo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kila kata nchini inakuwa na kituo cha afya kinachotoa huduma muhimu kwa wananchi.

“Fedha hizi ni matokeo ya dhamira ya dhati ya serikali kuboresha huduma za afya vijijini. Tunashukuru Serikali Kuu kwa kuendelea kuiwezesha Halmashauri yetu kutekeleza miradi mikubwa yenye tija kwa wananchi,” alisema Bi. Gumbo.

Aliongeza kuwa miradi hiyo itatekelezwa kwa kuzingatia taratibu zote za manunuzi na usimamizi wa fedha za umma, ili kuhakikisha thamani halisi ya fedha inaonekana katika matokeo ya miradi.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Songea, Dr Geofrey Kihaule alisema kukamilika kwa ujenzi wa vituo hivyo viwili kutasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Songea, na kuongeza kasi ya utoaji huduma hasa kwa akinamama wajawazito, watoto na wazee.

“Kupatikana kwa vituo hivi kutarahisisha upatikanaji wa huduma za afya ya uzazi, huduma za dharura, na maabara kwa wananchi waliokuwa wakitembea umbali mrefu kufuata matibabu,” alisema.

Wananchi wa kata hizo wamepokea kwa shangwe taarifa za fedha hizo, wakisema mradi huo utakuwa suluhisho la muda mrefu kwa changamoto ya upatikanaji wa huduma za afya karibu na makazi yao.

Bi. Janeth Mbawala, mkazi wa Kata ya Peramiho, alisema  “Tumehangaika kwa muda mrefu kutafuta huduma za afya mbali, hasa akina mama wajawazito. Tunashukuru serikali kwa kutuona na kutuletea kituo cha afya karibu.”

Naye Bw. Sospeter Mlelwa wa Kata ya Mpandangindo alisema “Kwa kweli hii ni neema kubwa. Vituo hivi vitapunguza gharama na muda wa kusafiri, hasa wakati wa dharura.”

Kwa mujibu wa taarifa kutoka idara ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ujenzi wa vituo hivyo umeshaanza kutekelezwa huku wananchi wakihamasishwa kushiriki katika hatua za awali za ujenzi kwa nguvu kazi.

Kupitia utekelezaji wa miradi hii, Serikali inaendelea kuthibitisha azma yake ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya kwa ukaribu, usawa na ubora unaostahili.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SONGEA DC YAHAMASISHA UMUHIMU WA LISHE BORA KWA WATOTO SHULENI

    November 27, 2025
  • FAHAMU KUHUSU BARAZA LA MADIWANI; MUUNDO NA UTENDAJIKAZI WAKE

    November 25, 2025
  • SONGEA DC, YATEMBELEA MIKOA INAYOLIMA KAHAWA KWA LENGO LA KUPATA UZOEFU

    November 19, 2025
  • DC NDILE AIPONGEZA HALMASHAURI YA SONGEA KWA KUIMARISHA HALI YA LISHE, ATOA WITO WA KUENDELEZA JITIHADA

    November 17, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa