• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

Tarehe ya Kuwekwa: October 23rd, 2025


Leo Oktoba 23, 2025, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Songea kimetembelea eneo la ujenzi wa stendi ya mabasi katika Kijiji Cha Parangu   inayotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii  (TASAF) ambao upo hatua za mwisho za ukamilishaji wake, mradi unaogharimu zaidi ya shilingi milioni 500 hadi kukamilika kwake 

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi. Hosana Ngunge, amesema ujenzi wa stendi hiyo ni moja ya miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na TASAF kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Songea. Alifafanua kuwa mradi huo unahusisha miundombinu muhimu kama matundu sita (6) ya vyoo, shedi nne (4), jengo la utawala, maduka 32 ya wafanyabiashara wadogo, pamoja na viunga vya maua vitakavyopamba eneo hilo.

“Kukamilika kwa mradi huu kutafungua milango ya kiuchumi kwa wananchi wa kata ya Parangu, Wananchi wataweza kufanya biashara zao kwa urahisi, wamiliki wa bodaboda na magari watapata fursa zaidi za kiuchumi, na suala la usafiri litakuwa jepesi kwani magari yatakuwa yanapaki moja kwa moja kijijini kwao,” alisema Bi. Ngunge.

Aliongeza kuwa mradi huo umezingatia vigezo vyote vya ubora na unatarajiwa kuwa kivutio kipya cha maendeleo kwa wananchi wa Parangu na maeneo jirani. Aidha, alisisitiza kuwa TASAF itaendelea kushirikiana na serikali za mitaa kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa inaleta matokeo chanya kwa walengwa wake.

Kwa upande mwingine, wananchi wa Kata ya Parangu wameelezea furaha na shukrani zao kwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuona umuhimu wa kuwaletea maendeleo kupitia mradi huo wa stendi.

Mwenyekiti wa kijiji cha Parangu, Bwana Ditram Ngonyani, akizungumza kwa niaba ya wananchi, alisema:

“Kuwa na stendi katika kata yetu ni ndoto ambayo hatukuamini kama ingeweza kutimia. Tunamshukuru sana Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na TASAF kwa kutuona sisi wananchi wa Parangu. Mradi huu ukikamilika, wananchi wa kijiji chetu, kata na hata vijiji jirani watapata fursa nyingi za kiuchumi. Tunasema asante kwa Serikali yetu ya awamu ya sita kwa kuendelea kuleta maendeleo hadi ngazi ya kijiji.”

TASAF katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea imekuwa ikitekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo yenye lengo la kuinua maisha ya wananchi, ikiwemo miradi ya afya, maji, ujenzi wa nyumba za watumishi, pamoja na utoaji wa ruzuku kwa kaya lengwa. Ujenzi wa stendi ya Parangu ni miongoni mwa miradi inayodhihirisha dhamira ya serikali katika kusogeza huduma karibu na wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa vijijini.

Kwa ujumla, mradi huu unatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo kwa Kata ya Parangu, kwa kuongeza mzunguko wa fedha, kuboresha huduma za usafiri, kuongeza ajira, na kuwapa wananchi fursa mpya za kujiletea kipato. Kukamilika kwake kutakuwa ni hatua kubwa katika safari ya kuinua uchumi wa wananchi wa Songea Vijijini na kuongeza mapato ya Halmashauri kupitia shughuli mbalimbali zitakazofanyika katika eneo hilo la stendi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SONGEA DC YAHAMASISHA UMUHIMU WA LISHE BORA KWA WATOTO SHULENI

    November 27, 2025
  • FAHAMU KUHUSU BARAZA LA MADIWANI; MUUNDO NA UTENDAJIKAZI WAKE

    November 25, 2025
  • SONGEA DC, YATEMBELEA MIKOA INAYOLIMA KAHAWA KWA LENGO LA KUPATA UZOEFU

    November 19, 2025
  • DC NDILE AIPONGEZA HALMASHAURI YA SONGEA KWA KUIMARISHA HALI YA LISHE, ATOA WITO WA KUENDELEZA JITIHADA

    November 17, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa