• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MKURUGENZI Songea Vijijini Ndugu Neema Maghembe asaini Mkataba wa Lishe.

Tarehe ya Kuwekwa: October 27th, 2022

MKUU wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Pololet Kamando Mgema ameongoza hafla fupi ya utiaji saini ya Mkataba wa usimamiaji wa afua za Lishe na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe.

Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mkurugenzi Lundusi-Peramiho ambayo imeudhuriwa na Watendaji Kata na baadhi ya wataalamu wa Halmashauri.

Akizungumza Mkuu wa Wilaya amesema suala la usimamiaji wa Mkataba wa Lishe limekua likifanyika kwa miaka mitano kuanzia ngazi ya Wizara, Mkoa, Wilaya, Kata hadi ngazi ya Kijiji hivyo lengo la Wilaya ni kuhakikisha inasimamia ipasavyo utekelezaji wa Afua za Lishe na kuchukua hatua madhubuti za kupunguza hali duni ya lishe.

‘’Rai yangu kwenu ni kwamba Mkataba huu utusaidie kubaini changamoto zilizopo katika maeneo yetu na kuchukua hatua madhubuti za kupunguza hali duni ya Lishe hususani udumavu wa watoto wenye umri chini ya miaka mitano ambayo ni asilimia 33 kwa mujibu wa tafiti ya Lishe Kitaifa ya Mwaka 2018’’, amesisitiza Mhe.Mgema.

Aidha amesema Halmashauri inatakiwa kufanya tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe mara nne kwa mwaka ili kuweza kutambua mwenendo wa utekelezaji wa afua za Lishe katika Kata na Vijiji pamoja na kutambua na kuzitatua changamoto ambazo jamii inayokutana nazo.

‘’Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anataka kukomesha Utapiamlo na udumavu wa akili kwa watoto ambao unasababishwa na lishe duni hivyo tunatakiwa kuboresha hali ya Lishe ili kupunguza athari hizo katika Halmashauri, Kata na Mtaa’’, amesema Mhe.Pololet.

Hata hivyo amewaagiza kila Mtendaji wa Kata ahakikishe anasimamia ipasavyo utekelezaji wa Lishe kwa kutembelea katika jamii kutafuta taarifa za hali ya Lishe kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano na kufanya ufuatiliaji kwa watoto ambao wameacha matibabu ya Utapiamlo kwa kushirikiana na wataalamu wa afya pamoja na kutoa elimu ya vyakula vya Lishe.

Pia amewataka Watendaji wa Kata kutembelea katika shule za msingi na kuhakikisha kwamba wanafunzi wanapata chakula na kushirikisha wanajamii juu ya athari ambazo mwanafunzi anaweza kukutana nazo juu ya ukosefu wa Lishe.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe amesema tathmini ya Lishe ni zoezi Mtambuka linalopaswa kutekelezwa na Viongozi na wananchi wanao wahudumia.

‘’Nipende kusema kwamba yote uliyoyasema Mkuu wetu wa Wilaya tumeyapokea na tunaenda kuyafanyia kazi ili kuhakikisha zoezi hili la kusimamia Lishe na Mikataba ambayo tumesaini tunaenda kuitekeleza kama vile yalivyo makubaliano ya Serikali’’, amesema Ndugu Neema.

Nae Afisa Lishe Wilaya Joyce Kamanga amesema katika jitihada za kuhakikisha wanaondoa janga la utapiamlo wakishirikiana na Viongozi wa Kata na Kijiji watatoa mafunzo kwa jamii na kuonesha kwa vitendo uaandaaji, upishi na matumizi bora ya vyakula vya lishe kwa wanajamii.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa