• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Mheshimiwa Jenista Mhagama Aungana na Wanakitongoji Wenzake Kujiandikisha Kwenye Daftari la Wapiga Kura.

Tarehe ya Kuwekwa: October 16th, 2024


Mbunge wa Jimbo la Peramiho na Waziri wa Afya, Mheshimiwa Jenista Mhagama, ameungana na wakazi wa kijiji cha parangu kitongoji cha Magigi katika kuhamasisha zoezi la wananchi kujisajili kwa ajili ya uchaguzi ujao. Akizungumza mbele ya hadhara, Mheshimiwa Mhagama aliweka msisitizo kuhusu umuhimu wa ushiriki wa wananchi katika kuchagua viongozi watakaowawakilisha kwenye serikali za mitaa na ngazi za juu zaidi.


"Wananchi mna nafasi ya kipekee ya kushiriki katika kujenga demokrasia ya taifa letu. Katika kipindi hiki, tutakuwa na uchaguzi ambao utahakikisha sauti zenu zinafika juu," alisema Mhagama. Aliwahimiza wale ambao bado hawajajisajili kuchukua hatua mara moja, akisisitiza kuwa hatua hii ni haki yao ya kikatiba na kidemokrasia.


Wakati akitoa pongezi kwa mafanikio yaliyopatikana hadi sasa katika zoezi la usajili, Mhagama alisema kuwa zaidi ya asilimia 50 ya wananchi katika Jimbo lake tayari wamejisajili, huku baadhi ya vitongoji  vikifikia asilimia 87.3 ya usajili.


"Ni muhimu sana kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi ili kuweza kuchagua viongozi wanaowajibika kuhakikisha maendeleo kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa," alisisitiza Mhagama. Pia aliongeza kuwa serikali imeweka utaratibu bora kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa njia huru na haki.


Kwa mujibu wa taarifa za sensa ya watu na makazi, kitongoji hicho cha Magigi kina idadi ya wakazi wapatao 48 ambao wanaotakiwa kujiandikisha, ambapo tayari wakazi 44 wameshajisajili, na hivyo kuwataka wale waliobaki kujiandikisha mapema.


Pia Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Wilaya ya Songea Thomas Masolwa, ametoa wito kwa wananchi wa Parangu na maeneo ya jirani kuendelea kumuunga mkono Mbunge wao katika safari ya kujiandikisha katika Daftari la Wapiga Kura. Akizungumza katika mkutano na wananchi, Masolwa alisisitiza umuhimu wa kujiandikisha kwa ajili ya kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi.


"Mbunge wetu ameungana nasi kuweka sahihi yake katika daftari hili, na safari yake imekuwa na umuhimu mkubwa kwa wananchi wote wa eneo hili. Tunaendelea kushikamana na kumsaidia katika hatua hii muhimu ya kuhakikisha haki ya kupiga kura inalindwa," alisema Masolwa.


"Ni kazi yetu sote kuhakikisha tunashiriki katika mchakato huu wa kujiandikisha na tunamuunga mkono mwakilishi wetu kwa nguvu zote," aliongeza Mwenyekiti Masolwa.


Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi Elizabeth Gumbo, ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Peramiho alibainisha kuwa jumla ya vituo 453 vimeandaliwa kwa ajili ya wananchi kwenda kujisajili na baadae kupiga kura , ambapo vituo hivyo vimehakikiwa na kuwekewa mawakala wa usimamizi wa uchaguzi. Kila kituo kitakuwa na mawakala wa vyama vya siasa ili kuhakikisha uwazi na uadilifu wakati wa mchakato wa kupiga kura.


Bi Gumbo pia alisisitiza umuhimu wa mawakala kutoka vyama vyote kuhakikisha kuwa wanalinda maslahi ya wananchi kwa kuchunguza kwa makini uendeshaji wa zoezi hilo. Alisema kuwa tayari kuna mawakala wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika vituo hivyo, kuhakikisha kila kituo kinaongozwa kwa uwazi na haki. Aidha, aliongeza kuwa jukumu la mawakala ni kuchukua tahadhari na kuzingatia sheria ili kuepusha migogoro yoyote itakayoweza kujitokeza.


Msimamizi huyo alihitimisha kwa kusema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Songea imejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa kila kituo kinasimamiwa kwa usahihi, na kwamba mawakala wamepewa maelekezo ya kina kuhusu taratibu za uchaguzi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KULA YAMEANZA SONGEA DC

    April 29, 2025
  • MHE . JENISTA MHAGAMA AZINDUA MADARASA 27 NA VYOO MATUNDU 44, SONGEA DC

    March 16, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa