• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MFUKO wa Maendeleo ya Jamii TASAF wanufaisha Songea DC

Tarehe ya Kuwekwa: October 10th, 2022

KATIBU tawala Wilaya ya Songea ndugu Pendo Daniel amewataka wananchi wa Songea vijijini kulinda miradi inayotekelezwa na mfuko wa maendeleo ya jamii wa TASAF.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Jimbo la Peramiho katika vijiji vya  Parangu na Mdunduwalo wakati wa kikao cha uzinduzi wa miradi.

"Nitoe rai kwa viongozi mliopo hapa nanyi mna jukumu la kuhakikisha kwamba mnasimamia mradi huu kwa weledi mkubwa ili  mradi ulete matunda tunayoyatarajia na mwisho kuondokana na kero ya kukosa mahitaji muhimu", amesisitiza ndugu Pendo.

Kwaupande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mheshimiwa Menas Komba amezitaka kamati zilizochaguliwa katika mkutano wa hadhara kuonesha uaminifu mkubwa katika kusimamia miundombinu ya ujenzi.

"Ninataka kuwasisitiza mnapokwenda kutekeleza mradi huu kila mmoja awe sehemu ya huu mradi kwa kushiriki vyema kwenye kusimamia na kulinda miundombinu na sio kuwaachia wanakamati pekee", amesisitiza Mhe.Menas.

Aidha Viongozi wote wameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama kwa kuweza kuleta fedha kiasi cha zaidi ya Milioni 395 kwaajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea ndugu Neema Maghembe ameahidi kushirikiana vyema na timu ya wataalamu, Waheshimiwa Madiwani wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Menasi Komba, kamati zilizoundwa na wananchi kwa ujumla ili kuhakikisha mradi  huu unakua wenye thamani halisi ya fedha iliyoletwa.

Akizungumza Afisa ufuatiliaji TASAF Wilaya Edwin Mlowe ambae amemwakilisha Mkurugenzi wa TASAF kutoka makao makuu amesema lengo la uzinduzi huo ni pamoja na kuzitambulisha kamati na kupeana majukumu ili kuanza kutekeleza miradi hiyo.

Amesema mradi wa TASAF umeleta fedha kiasi cha zaidi ya shilingi Milioni 225 kwa Kijiji cha Parangu sawa na asilimiili  90 kukamilisha mradi wa stendi ya mabasi, matundu ya vyoo manne  na maegesho ya magari pamoja na utengenezaji wa vigae.

 Pia Kijiji cha Mdunduwalo kimepokea fedha kiasi cha zaidi ya shilingi  Milioni 170 sawa na asilimia 90 kukamilisha mradi wa nyumba ya mganga wa hospitali ambayo ni mbili kwa moja, mradi wa uchimbaji wa kisima cha maji pamoja na matundu ya vyoo sita.

"Hizo asilimia 10 zinazobaki wanakijiji mnawajibu wa kujitolea na  kuzikamilisha kwa kushiriki shughuli mbalimbali Kama kuchimba msingi, kusogeza maji, mchanga, tofali na kushusha vifaa kutoka wenye gari hivyo nawaomba tuwape ushirikiano wa kutosha Serikali ya Kijiji na kamati iliyochaguliwa", amesisitiza Mlowe.

Wakizungumza wananchi wa Kijiji cha Parangu na Mdunduwalo wameishukuru Serikali ya awamu ya sita ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama na Mkuu wa Wilaya Mhe.Pololet Mgema kwa kuendelea kuwakumbuka na kuwapelekea fedha za kukamilisha miradi ya maendeleo.

Pia wamewashukuru Viongozi wa Chama wakiongozwa na Mhe.Menasi Komba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea ndugu Neema Maghembe na Viongozi wote wa ngazi ya Kata na Kijiji kwa kushirikiana nao vyema katika kuhakikisha miradi ya maendeleo inakamilika kwa wakati na viwango vinavyokubaliwa.

TASAF ni chombo cha Serikali ambacho kinasaidiana na vyombo vingine kinasaidia jitihada za kuondoa kero ya umaskini, upatikanaji wa maji safi na salama, elimu na afya ili kujenga jamii iliyo Bora.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa