• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MAANDALIZI KUELEKEA SIKU YA USAFI DUNIANI YAFANA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

Tarehe ya Kuwekwa: September 15th, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Songea kupitia kitengo cha usafi na mazingira kimefanya ziara katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa lengo la kuhamasisha shughuli za usafi wa mazingira ikiwa ni maandalizi ya maadhimisho ya siku ya usafi duniani itakayofanyika Tarehe 16/09/2023.

Halmashauri imechukua hatua hiyo  baada ya Tanzania na duniani kote kwa ujumla wakiadhimisha wiki ya usafi duniani ambapo kitaifa maadhimisho haya yanafanyika jijini Dodoma, Hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Songea ipo katika maandalizi ya siku ya usafi duniani ambapo inaadhimisha  kwa kuhamasisha jamii kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Akizungumzia taarifa hiyo Afisa mazingira wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Makisio Chengula amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika maeneo yote ya vijiji 56 ambavyo kamati hiyo ya usafi wa mazingira itakuwa inapita kufanya ukaguzi kwa kushirikiana na serikali za vijiji ambapo amesema.

"Kuna maeneo mengi katika Halmashauri yetu ya Wilaya ya Songea yanazalisha taka ngumu na laini lakini watu wamekuwa wakiziacha taka hizo zinazagaa maeneo mbalimbali na kupelekea uchafuzi mkubwa wa mazingira kwahiyo Halmashauri tumeunda kamati Maalumu ambayo itasimamia shughuli za usafi wa mazingira"

"Katika kufanikisha Zoezi hili kuna maeneo tumeyawekea kipaumbele katika kufanya usafi huo ikiwemo eneo la Hospitali ya Wilaya ya Songea iliyopo Mpitimbi, Hospitali ya mission Peramiho, vituo vya Afya vya Magagura, Matimira, Muhukulu, Liganga na Kilagano na Zahanati zote, maeneo ya stendi ya mabasi ambapo kwa hapa tutafanya stendi mpya (Peramiho), maeneo yanayofanyika  minada na maeneo ya Soko la Peramiho".( Namihoro). Hivyo niombe wananchi wa maeneo hayo kujitokeza kwa wingi kushiriki kufanya usafi na kutoa ushirikiano kwa kamati na Serikali za vijiji"

" Kilele cha maadhimisho hayo yatafanyika Tarehe 16/09/2023 katika Kijiji cha Lundusi ambapo ni  makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea hivyo tutahitimisha kwa kufanya usafi wa mazingira yote ya ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, hivyo niwaombe wananchi wa Kata  ya Peramiho hususani Kijiji cha Lundusi na maeneo ya jirani kujitokeza kwa wingi katika Kilele cha maadhimisho hayo Kinachotarajiwa kufanyika Tarehe 16/09/2023"

"Pia napenda kumshukuru  Mwenyekiti wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea kwa kutuwezesha kufanikisha zoezi hili muhimu na la Kitaifa" Alisema Makisio Chengula Kaimu Afisa Mazingira Wilaya.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa