Wizara ya Afya imetoa gari jipya kwa ajili ya kituo cha Afya Matimira, kilichopo kata ya Matimla, Halmashauri ya Wilaya ya Songea.
Gari hilo aina ya Land Cruser Hard Top lenye thaman ya Tsh. Milion 300, limekabidhiwa leo Juni 6,2025 kwa lengo la kuboresha huduma ya Rufaa kwa akina mama wajawazito na watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano.
Akilipokea gari hilo kutoka kwa Katibu wa Afya kwa niaba ya Mkurugenz mtendaji, Diwani wa kata ya Matimira, ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea amemshkuru Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuliona tatizo la akina mama wajawazito na watoto na kulipatia ufumbuzi.
Amemshkuru Mbunge wa Jimbo la Peramiho, ambaye pia ni Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama kwa kutimiza ahadi yake aliyowaahidi wananchi wa kata ya Matimira na vijiji vyake.
Aidha ametoa angaliza kwa Mganga mfawidhi kuhakikisha gari hilo linatumika kwa matumizi yaliyolengwa na si vinginevyo. Wananchi wa kata ya Matimira wameishukuru Serikali ya awamu ha Sita kwa kuwapatia Gari mpya ambayo itaokoa maisha ya watu wengi.
Halmashauri ya Wilaya Songea
Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea
Simu: 2602320 / 2602176
Simu ya mkononi:
Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz
Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa