• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

KAMATI YA SIASA MKOA WA RUVUMA YARIDHISHWA NA UJENZI SHULE YA SEKONDARI MPITIMBI

Tarehe ya Kuwekwa: October 11th, 2023

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma imeridhishwa na maendeleo ya miradi ya ujenzi katikati shule ya secondari Mpitimbi mnamo tarehe 9 Octoba 2023 wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na ilani ya Chama cha Mapinduzi katika Mkoa wa Ruvuma.

Kamati hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma Mhe. Odo Mwisho waliweza kukagua ujenzi wa vyumba 9 vya madarasa, vyoo matundu 14 na mabweni 4 ambayo fedha zake zimetoka Serikali kuu kwa awamu mbili chini ya Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan 

Akikagia miradi hiyo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma amewaomba wadau mbalimbali wa Chama na serikali kuwa na Imani na Chama cha Mapinduzi na kuendelea kumshika mkono Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa kwa kusimamia vyema fedha za miradi anazozitoa. Amesema

"Raisi wetu mama yetu mpendwa anahangaika huku na huku kutafuta fedha ili kuhakikisha mambo yanakwenda vizuri ndio maana  amekubali kutoa fedha za kutosha kujenga miradi hii katika shule hii ya Mpitimbi na sisi kama Kamati ya siasa ya Mkoa wa tumeridhishwa na mwendo mzuri pamoja na ubora wa ujenzi katika shule hii Rai yangu kwenu ni kuhakikisha miradi hii inatumika vizuri ili iweze kudumu kwa muda mrefu, pia nichukue fursa hii kuwaambia ninyi mlioko hapa tuendelee kuwa na Imani na Raisi wetu"

"Tumeona Madarasa yale tisa sehemu nyingine hakuna marumaru lakini nyinyi mmeweka safi kabisa Lakini pia madawati safi na mmeweka umeme kwakweli mnnastahili pongezi Lakini kitu kukubwa ambacho nampongeza Mkuu wa shule ya secondari Mpitimbi ujenzi wake unakwenda kwa wakati na kama tulivyosikia hapa kwenye taarifa tuliyo somewa anatarajia kukamilisha kabla ya muda aliopewa, lakini tumeona ujenzi ambao umestahili viwango vyote maana tumepita sehemu nyingine huko hawajafikia hatua kama hii lakini ni miradi inayofanana na hii lakini hapa  ubora tumeuona na unaridhisha, na ametuambia baada ya ujenzi huu kukamilika atabakiwa na akiba jambo ambalo mkuu wa shule anastahili pongezi kubwa sana"

Vilevile napenda kutoa Shukrani kwa Mhe Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuona umuhimu wa Elimu bora kwa watoto wetu na kuamua kutoa fedha hizo kujenga miundombinu hii ya kisasa katika shule hii, pia Shukrani zimfikie Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenista Joakim Mhagama kwa ufuatiliaji mzuri wa maendeleo ya Jimbo lake, pia Mwenyekiti wa Halmashuri, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Songea na timu yake kwa ujumla, Balaza la Madiwani na viongozi wote wa Chama Cha Mapinduzi kuanzia ngazi ya Kijiji mpaka Mkoa kwa kuhakikisha ilani ya Chama cha Mapinduzi inatekelezwa vyema.

Mkuu wa shule ya sekondari Mpitimbi akisoma taarifa ya fedha zilizopokelewa  kwaajili ya utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu katika shule ya sekondari Mpitimbi amesema walipokea jumla ya shilingi 879,800,000.00, kwaajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa9, mabweni 5 na matundu ya vyoo14, kutoka Serikali Kuu na SEQUIP. Na Hadi sasa Madarasa 6 yamekamilika na yanatumika na 3 hatua ya ukamilishaji, huku matundu 14 ya vyoo yamekamilika, pia bweni 1 limekamilika na linatumika na 3 yapo katika hatua ya ukamilishaji.

Nae aliweza kutoa Shukrani kwa Mhe Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwapa fedha hizo ili kujenga miundombinu ya kisasa, pia, Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenista Joakim Mhagama kwa msaada wake wa hali na mali, pia Chama cha Mapinduzi kuanzia ngazi ya Kata hadi Mkoa kwa ufuatiliaji mzuri wa miradi hii pia Diwani wetu kwa kushirikiana nasi bega kwa bega na kamati nzima ya ujenzi kwa kuhakikisha mradi huu unakamilika.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa