• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

IDADI ya wananchi kuripoti vitendo vya rushwa TAKUKURU yaongezeka

Tarehe ya Kuwekwa: April 28th, 2021

Kaimu Kamanda wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa wa mkoa wa Ruvuma Owen Jassoni amesema idadi ya wananchi wanaotoa taarifa dhidi ya vitendo vya rushwa imeongezeka toka  wastani wa watu  75  hadi 131 kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi 2021.

Jassoni ameyasema hayo wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi kwa waandishi wa habari katika ukumbi wa ofisi za Taasisi hiyo Manispaa ya Songea hivi karibuni.

Jassoni emesema ongezeko hilo limetokana juhudi za Taasisi hiyo kuwajengea uwezo wananchi kuhusu madhara ya vitendo vya rushwa katika jamii kupitia makongamano,uanzishwaji wa clabu za wapinga rushwa kwenye shule za msingi na sekondari,machapisho na TAKUKURU inayotembea huduma ambayo  watumishi wa Taasisi huwafikia wananchi kwenye makazi yao.

 Ameongeza kwakusema kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi Taasisi imefanikiwa kufanyakazi mbalimbali kama ukaguzi wa miradi ya maendeleo,kutatua changamoto za wananchi dhidi ya kudhulimiwa haki zao,ufuatiliaji wa ruzuku wa fedha za TASAF na kuwafikisha mahakamani waliobainika kuhusika na vitendo vya rushwa.

Jassoni amesema Taasisi hiyo itaendelea na kazi ya kutoa elimu kwa wananchi kwa lengo la kuimarisha uelewa na uwezo wa wananchi kupambana  na kupinga vitendo vya rushwa ambavyo  vinasababisha ukosefu wa haki na na dhuluma katika jamii.

Jassoni ameitaja mikakati ya utendaji kazi kwa kipindi cha mwezi Aprili hadi Juni  ni pamoja na kufuatilia shughuli za miradi ya maendeleo ili thamani fedha ilingane na miradi,itaendelea kutoa elimu ya kupiga vita vitendo vya rushwa na wananchi kuwa tayari kutoa ushahidi pale wanapotakiwa kufanya hivyo sanjari na kuendelea na uchunguzi wa makosa ya rushwa na kuchukua hatua stahiki.

Jassoni ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuendelea kushirikiana na Taasisi hiyo kukemea, kutoa taarifa za vitendo vya rushwa na kukataa rushwa kwakufanya hivyo mapambano dhidi ya rushwa yatafanikiwa katika jamii.

”sote kwa pamoja tuikatae rushwa”

Imeandaliwa na kuandikwa

Jacquelen Clavery

Afisa Habari

 Songeadc 

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa