• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Halmashauri ya Wilaya yatoa Mafunzo ya mifumo ya FFARS na PlANREP kwa watumishi.

Tarehe ya Kuwekwa: September 25th, 2017

Halmashauri ya wilaya ya Songea imetoa mafunzo ya mfumo wa FFARS na Planrep kwa wataalamu wake ili waweze kuitumia mifumo hiyo kwa ufanisi. Mafunzo hayo yamefanyika kuanzia tarehe18/09/2017. Mpaka tarehe 22/09/2017.  Wataalamu hao kwa  sasa wanamudu kuitumia mifumo hiyo kwa ufanisi mkubwa.

Akifungua mafunzo hayo Afisa Mipango wa Halmashauri ya wilaya  ndugu Shaban Millao amewataka wataalam hao kutumia vizuri muda wa mafunzo ili waweze  kuitumia kwa ufanisi na ilete tija kwa Halmashauri ya Wilaya ya Songea na Taifa kwa ujumla. Amesema malengo  makuu ya serikali ni kuhakikisha mifumo hiyo inatumika ili kupunguza gharama zisizo za lazima katika uandaaji wa bajeti za Halmashauri na utoaji wa taarifa za kifedha kwa vituo vya kutolea huduma.

Afisa Tehama wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea ndugu John Luoga amewataka kutumia mifumo hiyo kwa uangalifu na umakini pamoja na kuzingatia taratibu kwani mifumo hiyo haifuti  taratibu zinazotumika kwa sasa bali inarahisisha upatikanaji wa taarifa na kupunuza matumizi ya karatasi.

Mafunzo hayo yalitolewa na wataalamu wa ndani waliopatiwa mafunzo ya mifumo hiyo Mkoani Mtwara mwezi Julai 2017. Wataalam hao ni Afisa Mipango ndugu. Shaaban Millao, Afisa Tehama ndugu. John Luoga, Mganga mkuu wa Wilaya ndugu. Yesaya Mwasubila, Katibu wa Afya ndugu Sixmund Maseti  na Mhasibu Blandina Kimaro. Mafunzo hayo yameendeshwa kwa siku tano na yametolewa kwa washiriki 184 kutoka katika Idara, vitengo na Vituo vya kutolea huduma kwa jamii.

Mfumo wa Planrep ni mfumo ulioboreshwa kutoka kutumika katika kompyuta pekee na kufikia kutumika katika mtandao wa intaneti. Mfumo huo utapunguza gharama kubwa za uandaaji wa bajeti za halmashauri na kuwezesha kutuma bajeti hizo mkoani na baadae wizarani kupitia mfumo huo.

Mfumo wa FFARS ni mfumo wa utoaji taarifa za kifedha kwa vituo vya kutolea huduma kama  shule za msingi, shule za sekondari , zahanati na vituo vya Afya. Watumiaji wa mfumo huu wataweza kuandaa taarifa za kifedha watakazokuwa wanazitumia kwa shughuli mbalimbali katika vituo vyao.

Mafunzo hayo kwa  wakuu wa Idara na vitengo  na wasaidizi  wao,  wakuu wa shule, pamoja na wakuu wa vituo vya afya na zahanati yalifungwa na Kaimu Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Wilaya ndugu Tanu Kameka.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KULA YAMEANZA SONGEA DC

    April 29, 2025
  • MHE . JENISTA MHAGAMA AZINDUA MADARASA 27 NA VYOO MATUNDU 44, SONGEA DC

    March 16, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa