• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

DC Ndile akagua miradi ya ujenzi Songea DC

Tarehe ya Kuwekwa: June 24th, 2023

MKUU wa Wilaya ya Songea Mhe. Kapenjama Ndile amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya BOOST na SWASH inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Ziara hiyo imefanyika tarehe 23 Juni 2023 ambapo aliambatana na Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Neema Maghembe Pamoja na timu ya Wataalamu.

Mhe. Ndile akiwa katika ziara hiyo amekagua ujenzi wa mradi wa BOOST wa vyumba viwili vya madarasa na matundu matatu ya vyoo katika shule ya msingi Matama ambapo mradi unatekelezwa kwa fedha kiasi cha shilingi Milioni 53.1 kutoka Serikali kuu.

Pia Mhe. Ndile amekagua ujenzi wa mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya shule za masingi na Awali (BOOST) wa vyumba viwili vya madarasa na matundu matatu ya vyoo katika shule ya msingi Nakawale unaotekelezwa kwa fedha kiasi cha shilingi Milioni 53.1 kutoka Serikali Kuu.

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya amekagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa ya Awali ya mfano na matundu ya vyoo katika shule ya msingi Humbaro unaotekelezwa kwa fedha kiasi cha shilingi Milioni 66.3.

Vilevile amekagua ujenzi wa mradi wa SWASH wa ujenzi wa vyoo matundu 13 katika shule ya msingi Lihuhu unaogharimu fedha kiasi cha shilingi Milioni 33,743,862 pia ujenzi vyoo matundu 14 katika shule ya msingi Lung‘oo unaogharimu fedha kiasi cha shilingi milioni 36,193,862.

Mradi mwingine uliokaguliwa ni Pamoja na mradi wa ujenzi wa vyumba tisa vya madarasa, mabweni manne na vyoo matundu 14 katika shule ya sekondari Mpitimbi ambao unatekelezwa kwa fedha kiasi cha shilingi Milioni 751.8 kutoka Serikali kuu ambao una lengo la kuongeza miundombinu ya wanafunzi wa kidato cha tano.

Akizungumza katika ukaguzi wa miradi hiyo amesisitiza miradi ikamilike ndani ya muda uliopangwa na kwa viwango na ubora unaokubalika na Serikali.

‘‘Viongozi wote mnaohusika na miradi hii jitahidini kutoa hamasa kwa wananchi pale ambapo nguvu za wananchi zinahitajika waweze kushiriki kikamilifu miradi iweze kukamilika kwa wakati’’, amesisitiza Mhe. Ndile.

Akihitimisha ziara hiyo Mkuu wa Wilaya amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha hizo za kuboresha miundombinu ya Elimu, pia ametoa rai kwa walimu wa shule kuhakikisha wanafanya jitihada za kupandisha ufaulu kwa wanafunzi kama shukrani kwa Mheshimiwa Rais.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa