• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

VIONGOZI wa Taasisi watakiwa kuheshimu misingi ya utawala bora

Tarehe ya Kuwekwa: September 2nd, 2021

Viongozi wa Taasisi mbalimbali wamekumbushwa kuheheshimu misingi ya utawala bora pindi wanapotoa huduma kwa waliowapa dhamana kwakufuata taratibu,kanuni na sheria za nchi.

Kauli hiyo imetolewa na Mwezeshaji na Mshauri Mwelekezi Utawala Bora Wakili Lawrence Chuma katika warsha ya Utawala Bora iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma hivi karibuni.

Wakili Chuma amesema Viongozi wa Taasisi mbalimbali wametakiwa kuzingatia sheria,kaninu na taratibu za utawala bora na  uwajibikaji katika kuwatumikia wananchi kwalengo la kuwajengea wananchi misingi imara ya kuwabijika na kushiriki kuijenga nchi yao.

“Viongozi mmepata dhana ya kuongoza wananchi hivyo mnapaswa kuzingatia misingi ya utawala bora kwa kutoa taarifa sahihi na kwakutumia lugha nyepesi ambayo itawezesha wananchi kuwa na uelewa”.amesema Wakili Chuma.

Wakili Chuma ameongeza kwa kusema utawala unaozingatia demokrasia,uwajibikaji,ushirikishwaji, maridhiano,haki za binadamu na utawala wa sheria unatoa fursa kwa wananchi kunufaika na rasilimali za nchi kwa pamoja.

Kwa upande mwingine Wakili Chuma amewataka wananchi kuwajibika kikamilifu katika swala zima la kulinda,kusimamia na kutunza rasilimali za nchi ili ziweze kutoa huduma endelevu kwa vizazi vijayo.

Kwa upandewake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika lisilo la kiserikali Millenium Art Group Mnung’a Shaibu Mnung’a ametoawito kwa viongozi kuwajibika kwa wananchi kwa kuwapa taarifa sahihi kwakuitisha mikutano ya hadhara ambayo inatoa fursa kwa wananchi kujadiliana na kuamua kwa pamoja katika kutekeleza mipango yao.

 “Tunasisitiza sana viongozi kuitisha mikutano ambayo hailengi tu kuwapa taarifa wananchi kuhuhsu michango na maelekezo mbalimbali “amesema Mnung’a

Amesema wananchi wamekata tamaa ya kwenda kushiriki mikutano ya hadhara kwakujenga dhana ya kwamba kwenye mikutano hiyo agenda ni kupatiwa taarifa za michango mbalimbali na maagizo ya jambo fulani.

Kufuatia hali hiyo Mnun’ga ametoa wito kwa viongozi wa taasisi mbalimbali kuwajibika kutoa elimu kwa wanachi katika kuwashirikisha na kujadili kwa pamoja mipango inayopangwa na serikali na utekelezaji wake ili wananchi nao washiriki kikamilifu.

Millenium  Art Group Shirika lisilokuwa la kiserikali limeendesha mafunzo kwa Wakuu wa Idara na Vitengo mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea ambao nao wanatakiwa kuzingatia misingi ya Utawala Bora.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa