• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea imefanikiwa kupunguza ukubwa watatizo la malaria hadi asimia 15.1

Tarehe ya Kuwekwa: November 16th, 2020

Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma imefanikiwa kupunguza ukubwa wa tatizo la ugojwa wa malaria hadi kufikia asilimia15.1 kutokana na mbinu na mikakati ya kupambana na ugonjwa huo ilivyotekelezwa kwa uweledi mkubwa.

Mratibu wa malaria wa Halmashauri hiyo LEAH MHALULE ameitaja mbinu na mikakati waliyoitumia katika kupambana na tatizo hilo kuwa ni kuelimisha jamii kuhusu matumizi bora ya vyandarua kupitia kampeni ya kitanda kwa kitanda, kudhibiti mazalia ya mbu kwa kupulizia dawa ya viuawadudu wanaosababisha vimelea vya malaria,

Mikakati mingine ni pamoja na matumizi ya dawa ya SP kwa akina mama wajawazito sambamba na kuwagawia nyandaru mara wanapoanza kliniki ,ugaawaji wa vyandarua mashuleni na Watoto wenye umri wa miezi tisa .

Mhalule ametoa wito kwa kila kaya kutumia chandarua wakati wa kulala na kuto puuza matuzi ya chandarua kwa sababu chandaru ni kinga namba moja katika kupambana na maambukizi ya vimelea vya malaria na matumizi ya dawa ya SP kwa wajawazito.

“Viongozi wa Serikali na wadau wa kupambana na malaria wekeni agenda ya Elimu ya kupambana na malaria kuwa ya kudumu katika vikao kama UKIMWI nia ikiwa kupambana na kutokomeza ugonjwa wa malaria, na malaria kuwa historia katika jamii”,amesema Mhalule.

Mhalule amesema kwa kipindi cha mwaka 2017,2018, ukubwa wa tatizo la malaria ulikuwa wastani wa asilimia 58 ukilinganisha na mwaka 2020 hadi kufikia mwezi Septemba ukubwa wa tatizo la ugonjwa malaria ulishuka mpaka kufikia  asilimia 15.1

Kwaupande wake Afisa Afya wa Wilaya hiyo JOHN KAPITINGANA amesema kuelekea msimu wa mvua Wilaya imepokea dawa za viuawadudu lita 640 kutoka wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na wototo kwa ajili ya kupuliza kwenye mazalia ya mbu katika vijiji 10 ambavyo vina idadi kubwa ya maabukizi ya vimelea vya malaria ukilinganisha na vijiji vingine.

Amewashukuru wananchi wamekuwa na mwitikio chanya kwa kutoa ushirikiano katika kufanikisha kampeni na upuliziaji wa dawa na kuiomba Serikali kuongeza ujazo wa dawa za viuawadudu kwa sababu iliyopokelewa haikidhi mahitaji ya kuvifikia Vijiji vyote 56 vya Wilaya hiyo.

Kapitingana amevitaja Vijiji vilivyopata kipaumbele kufuatia ukubwa wa tatizo  kuwa ni Peramiho A na B, Mpitimbi A na B, Litowa  Parangu,Muhukuru Lilahi na Barabarani,Namatuhi na Nakahuga.

Ametoa wito kwa wananchi kufika katika vituo vya kutolea huduma za Afya kwa maana ya Zahanati Vituo vya Afya na Hosiptali kwa uchunguzi na tiba mara wanapo hisi homa badala ya kujitibia majumbani pasipo kufanyiwa uchunguzi.

Ugonjwa wa malaria bado ni tisho kwa afya ya binadamu na Mkoa wa Ruvuma ni wa 5 kitaifa kwa ukubwa wa tatizo la malaria kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2017 zilizotolewa na shirika la Takwimu (NBS) Tanzania.

 

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa