• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya

YALIYOJILI katika kikao cha Baraza cha robo ya tatu Januari-Machi 2023 Songea DC

Tarehe ya Kuwekwa: May 14th, 2023

KIKAO cha baraza la Madiwani cha robo ya tatu Halmashauri ya Wilaya ya Songea kimefanyika katika ukumbi wa mikutano Lundusi-Peramiho Mei 13 2023 . Kikao hicho kimeudhuriwa na Katibu Tawala, Waheshimiwa Madiwani, Wakuu wa Idara na Vitengo, Viongozi kutoka taasisi mbalimbali kama TRA, TAKUKURU, kamati ya Usalama ya Wilaya Pamoja na Watendaji wa Kata.

Lengo la kikao hicho ni kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo yahusuyo Halmashauri ya Wilaya ya Songea katika Nyanja mbalimbali, vilevile ni Pamoja na kupokea taarifa za utekelezaji wa kamati mbalimbali kwa kipindi cha robo ya tatu ya Januari-Machi 2023.

Akizungumza Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Simon Kapinga Kwa niaba ya Madiwani alitumia nafasi hiyo kuipongeza na kuishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Daktari Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama Kwa kuendelea kutoa fedha nyingi za miradi jambo ambalo linaleta faraja Kwa wananchi kwa kusogezewa huduma muhimu karibu na maeneo yao.

Aidha, katika baraza hilo Makamu Mwenyekiti alitoa rai kwa Afisa Ushirika na wataalamu kuhakikisha wanafuatilia kwa umakini Vyama vya Ushirika ambavyo wananchi wanavitumia kuuzia mazao yao katika mfumo wa stakabadhi ghalani kuhakikisha havina madeni ili wananchi waweze kuuza mazao yao na kupata fedha zao moja kwa moja.

Pia Katika kikao cha baraza la Madiwani cha robo ya tatu ya Januari-Machi 2023 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe aliishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama  kwa kutoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo.

Vilevile amewashukuru Waheshimiwa Madiwani, Viongozi wa Chama, Timu ya Wataalamu Pamoja na Watendaji wa Kata na Vijiji kwa kuendelea kushirikiana, pia amewasisitiza kuendeleza ushirikiano huo katika kutekeleza na kusimamia shughuli za maendeleo ili Halmashauri isonge mbele Zaidi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO October 12, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • TIMU ya Wataalamu yafanya ufuatiliaji wa miradi Songea DC

    May 27, 2023
  • Timu ya Wataalamu yafanya ufuatiliaji wa miradi ya ajira ya muda inayotekelezwa na Walengwa wa TASAF.

    May 27, 2023
  • YALIYOJILI katika kikao cha Baraza cha robo ya tatu Januari-Machi 2023 Songea DC

    May 14, 2023
  • YALIYOJILI katika kikao cha utekelezaji wa tathmini ya Afua ya Lishe robo ya tatu Songea DC

    May 08, 2023
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa