• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

"WEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI ILI KUJENGA TANZANIA YA VIWANDA"

Tarehe ya Kuwekwa: October 17th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Songea Wilmani Kapenjama Ndile amewataka wanawake wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea kishikamana na kufuata taratibu za vikundi vyao ili waweze kukua kiuchumi. Ameyasema hayo wakati akizungumza na wanawake wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea kwenye uzinduzi wa jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi ambapo Kiwilaya umefanyika tarehe 16 octoba 2023 katika ukumbi wa Mama Mkuwa Namihoro Peramiho.

Pia Mkuu wa Wilaya ya Songea amewashauri wanawake wengine ambao walinufaika na mikopo isiyokuwa na riba ambayo ilitolewa kupitia Halmashuri ya Wilaya ya Songea kuweza kurejesha mikopo hiyo ili na wengine waweze kunufaika. Amesema.

"Zamani wanawake walichukuliwa kama viumbe dhaifu sana hata walipokuwa wakianzisha vikundi vyao ilikuwa ni rahisi kuvunjika kwasababu ushirikiano ulikuwa mdogo kwahiyo vikundi vyao vilivumjika kwasababu vilikosa nguvu, lakini kwa sasa mambo yamebadilika wanawake mmetawala kila upande na mkiaminiwa mnaweza sasa kupitia jukwaa hili kwenye vikundi vyenu mnatakiwa kujenga misingi imara ili kufanya kikundi chenu kusonga mbele hususani kwenye masuala ya muda, watu wengi Wanafeli mambo yao kwasababu ya kutozingatia muda kwahiyo niwaombe wanawake mliopo hapa na wengine huko kuzingatia taratibu zote mnazojiwekea kwenye kikundi ".

"Pia katika risala iliyosomwa hapa nimesikia kuna baadhi ya vikundi havijarejesha marejesho yao jambo ambalo linakwamisha maendeleo ya wengine kwasababu Raisi wetu anania njema na wananchi wake ndiomaana alitoa fungu kwaajili ya kuwezesha vile vikundi sasa kama kunawengine hawajarejesha tunamvunja moyo Raisi wetu kwahiyo nichukue fursa hii kuwaomba wote ambao hawajarejesha  mikopo warejeshe ili na wengine wanufaike" alisema Kapenjama Ndile Mkuu wa Wilaya ya Songea.

Nae Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Bi. Zawadi Nyoni ametoa Shukrani zake kwa Mkuu wa Wilaya ya Songea kwa kuitikia wito wa kuja kuwazindulia jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi ambapo pia amewaomba wanawake waliohudhuria kwenye jukwaa hilo kuwa mabalozi kwa wanawake wengine kwa kuyatendea kazi yale yote yaliyosemwa pale. Ambapo uzinduzi huo umeenda na Kaulimbiu isemayo WEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI ILI KUJENGA TANZANIA YA VIWANDA

Pia pamoja na mambo mengine wanawake wa Songea wamepata mafanikio kadha wa kadha kutokana na shughuli zao za kiuchumi kupitia vikundi vya wanawake pia wanafursa ya kuwezeshwa mikopo kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo hutenga asilimia 4 kwaajili ya utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, ambapo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya kiasi cha shilingi 86,103,944.00 ilikopeshwa kwa vikundi 14 vya wanawake na mwaka 2022/2023 jumla ya shilingi 66,241,815.11 zilikopeshwa kwa vikundi 10 vya wanawake. Hivyo jumla ya shilingi 152,345,759.11 imekopeshwa kwa vikundi 24 vya wanawake kwa kipindi cha miaka miwili ya fedha.

Mikopo hiyo Haina riba ambapo imesaidia sana kuinua mafanikio ya wanawake baadhi ya mafanikio hayo ni pamoja na vikundi vya wanawake kujiimariaha kimiradi kama vile ufugaji wa kuku, kilimo cha mbogamboga, uoteshaji wa uyoga, kilimo cha mahindi, ufugaji wa nyuki na viwanda vidogovidogo vinavyozalisha bidhaa mbalimbali kama vile mikate.

Pamoja na mafanikio wanayoyapata wanawake hao wajasiliamali wameeleza changamoto wanazokutananazo ikiwa ni pamoja na kufanyiwa vitendo vya ukatili, kukosa mitaji mikubwa ya kuweza kuendeleza shughuli zao za kiuchumi, kukosa haki ya kumiliki ardhi hususani wanawake wanaoishi vijijini, pia wanakosa masoko ya bidhaa wanazozizarisha, kukosa haki ya kumiliki uchumi na kipato cha Kaya, pia kutelelezwa na watoto.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa