• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WAZIRI Jenista awataka wananchi kutunza miundombinu ya Maji

Tarehe ya Kuwekwa: July 19th, 2023

Mbunge wa Jimbo la Peramiho na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama ametembelea na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji katika Kijiji cha Peramiho A.

Akizungumza Mheshimiwa Jenista amewasisitiza wananchi kutunza na kulinda miundombinu ya mradi huo wa maji ili uendelee kuwanufaisha.

“Kukamilika kwa mradi huu ambao umefikia asilimia 98 utasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa tatizo la uhaba wa maji ambalo limekuwa likiwasumbua kwa mda mrefu hivyo tuna kila sababu ya kumshukuru Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea fedha hizo”, amesisitiza Mheshimiwa Jenista.

Akisoma taarifa Mhandisi wa maji Wilaya Triphon Mwanangwa amesema mradi hadi kukamilika utagharimu fedha kiasi cha shilingi milioni 285 kutoka Serikali Kuu.

“Lengo la mradi ni kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wa vijiji vya Peramiho A na Nguvu moja ambao walikuwa wanapata maji kwa mgawo kwa kuwa tanki lililokuwa linatumika lilikuwa ni dogo (lita 65,000) tu ukilinganisha na mahitaji ya maji kwa wananchi”, amesema Mhandisi Mwanangwa.

Aidha, Mhandisi ameongeza kuwa mradi huu unatekelezwa kwa fedha za P for R (Payment for Result) yaani Lipa kwa matokeo ambapo kukamilika kwa ujenzi huu watu wapatao 6,267 watanufaika na huduma ya maji.

Chanzo cha maji ni chemichemi za asili chenye uwezo wa kuzalisha lita 133,000 kwa siku na uwezo wa pampu ni lita 17,000 kwa saa.

Wakizungumza wananchi wa Kata ya Peramiho wamemshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta fedha za kutekeleza mradi huo wa maji.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO October 12, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SIKU CHACHE ZATOLEWA MIFUGO ILIYOINGIZWA KINYEMELA IONDOLEWE KIJIJI CHA LIANGWENI.

    November 23, 2023
  • MKUU WA MKOA RUVUMA; "VIONGOZI WA KIMILA TUMIENI MAMLAKA YENU KUDUMISHA MILA NA DESTURI ZETU".

    November 22, 2023
  • DKT. CHARLES MSONDE ARIDHISHWA NA UBORA WA UJENZI SEKONDARI MAPOSENI.

    November 22, 2023
  • Dkt. Kaijage aipongeza Awamu ya Sita kwa kuwajali Watumishi

    November 13, 2023
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa