• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WANANCHI WANUFAIKA UPATIKANAJI WA HATI ZA VIWANJA KWA URAHISI

Tarehe ya Kuwekwa: September 27th, 2022


Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, wamesogezewa huduma katika eneo lao, ili waweze kupata Hati ya kumiliki viwanja pia kupata utatuzi wa migogogro ya Ardhi ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Huduma hii itakayodumu kwa siku tatu, yaan Jumanne, Jumatano na Ijumaa imekua msaada sana kwa wakazi wa jimbo la Peramiho na kata zake. Zoezi la kusikiliza malalamiko ya wananchi kuusu masuala mbalimbali yanahusiana na viwanja pamoja na umiliki, limekua likifanyika, lakin kwa sasa limeboreshwa, ili kuhakikisha kero hii inakwishwa kwa asilimia zote.

Akizungumza Kamishna msaidizi wa Ardhi mkoa wa Ruvuma Ngd. Saidi Juma Kijiji amesema “  leo tupo kwenye zoezi letu la kawaida, zoezi la kusikiliza malalamiko kwa wananchi. Tumejiwekea utaratibu huu baada ya Mhe. Waziri kutoa maelekezo ya siku miamoja ya kushughulikia malalamiko yote yanayohusiana na maswala ya Ardhi. Tulianza wiki iliyopita katika manispaa ya Songea, lakin leo tupo Halmashauri ya Songea na tutakuwepo kwa siku tatu”

“Zoezi kubwa  ni; moja kushughulikikia malalamiko yote yanayohusiana na ardhi kwenye Halmashauri ya Songea lakini pili ni kutoa Hati za papo kwa papo kumbuka sekta za ardhi zote zipo hapa kwaajili ya kushughulikia  na shughuli mbalimbali au changamoto mbalimbali zinazohusiana na maswala ya Ardhi”

“Maelekezo aliyoyatoa Mhe. Waziri ni pamoja na utoaji wa Hati kwa wakati, na ikumbukwe pia gharama za upatikanajini wa Hati zimepungua ambapo ukiwa na shilingi elfu hamsini unaweza kupata Hati kwa kiwanja kimoja, ambayo ni nusu ya gharama za awali”.

Aidha ofisi ya msajili wa hati, ni miongoni mwa ofisi zilizofika Halmashauri ya Songea lengo ikiwa ni kuhakikisha wananchi wanatambua umuhimu wa utunzaji wa nyaraka,  pia namna ya kufanya kama umeuza ama umenunua kiwanja ili kuweka majina yako na  kuepuka migogoro kwa baadae.

Christina Daniel Nyerere, Msajili wa Hati Msaidizi Mkoa wa Ruvuma anasema “ kunachangamoto mwananchi anaweza kuipata kama hatofanya miamala inayopatikana kwenye ofisi ya Msajili wa hati ikiwemo kwenye kubadilisha majina, ama  umeuza kiwanja chako umemuamishia mtu mwingine, Yule mtu asipofanya mabadiliko kwa wakati itamgarimu kwanza, atakiendeleza bila kufanya mabadiliko kwa wakati itamgharimu kwanza atajikuta analipa gharama kubwa serikalini tofauti angefanya kwa wakati”

Dicksoni Emmanueli, ni mpima Ardhi wa Mkoa wa Ruvuma, kwa nafasi yake nae alikua na haya ya kusema “ leo tupo hapa kwa sababu,  huu mji mdogo wa Peramio tulishapima viwanja zaidi ya 2300, lakini kabla ya hapo kulikua na viwanja 2000,  pamoja na kupima lakini bado  mwamko wa wananchi kuja  kumilikishwa viwanja umekua mdogo sana, hivyo tunapokua na viwanja vingi vimepimwa lakini havijamilikishwa inakua haina faida ya upimaji, hivyo basi  ili kuwasaidia wananchi wajue umuhimu wa kupimiwa ni lazima pia wawe na nyaraka”

“Si hilo tu, tumekuja kuwahamasisha wananchi kwakuwa hata gharama za upimaji zimepungua, mwaka jana walikua wanalipa laki moja na hamsini lakin kwa sasa ni shilingi elfu hamsini, hivyo mwananchi ambaye alipimiwa aje amilikishwe kwa sababu gharama zimeshushwa. Watu wasiendelee kujenga maeneo ambayo hayajapimwa”

“Hili ni zoezi la kimkakati, ikizingatia tuna mpango wa kutoa Hati miliki zaidi ya Mia Tatu  (300) kwa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ambalo linawekwa katika umuhimu wa kulinda umiliki pamoja na kuondoa  migogoro. Tunaendelea kutoa wito kwamba zoezi hili ni endelevu na tutaendelea kufikia wananchi wote katika maeneo mbalimbali”. Alisem Saidy Mrisho Msananga, Afisa Ardhi Mteule Halmashauri ya Wilaya ya Songea

Wanachi wemeshukuru Serikali, Waziri  pia mkoa na Halmashauri kwa kuwafikishia huduma hii karibu nao, namna wanavyotatiua migogoro inayohusiana na Ardhi  pia kuwarahisishia namna ya kupata hati.

Theresia Msuya, mkazi wa kijiji cha Peramiho A, amesema “ tunashukuru sana hili zoezi linaloendelea kwani kwa upatikanaji wa Hati utanisaidia kwa mambo mengi sana, ikiwa ni pamoja na kupata Mkopo lakini pia inaweza kutumika kama dhamana. Zamani haikua rahisi hivi kilikua ni kitu kigumu sana kupata Hati, ila kwa sasa Serikari imerahisisha kwa kuleta kijijini kwetu. Nawashkuru viongozi wote wa wilaya, Mkoa Taifa kwa kuona wananchi wengi wanapata shida kupata hati na sasa wameturahisishia.



Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI 28 VAPATIWA MIKOPO YA TSH MILIONI 249 NA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    July 03, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

    July 01, 2025
  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa