• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

UKAGUZI WA MIRADI WAENDELEA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

Tarehe ya Kuwekwa: October 27th, 2023


Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea inayoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashuri Mhe. Menas Komba imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea

Miradi iliyokaguliwa ni pamoja na ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Magima iliyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi hivyo serikali ikapeleka kiasi cha shilingi milioni 50 kwaajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa Zahanati hiyo na mpaka sasa kiasi kilichobaki ni shilingi 60,55,000 huku ujenzi ukiwa kwenye hatua za ukamilishaji.

Pia kamati hiyo iliendelea na ziara katika shule ya Msingi Parangu iliyoko Kijiji cha Parangu ambapo kamati ilikagua mradi wa SWASH matundu 15 ya vyoo ambapo shule hiyo ilipokea kiasi cha shilingi 37,643,862.66 kwaajili ya ujenzi wa matundu 15 ya vyoo na mpaka kamati hiyo inakagua mradi huo tayari umkwisha kamilika.

Kisha kamati ya Fedha ilielekea katika Kijiji cha Kilagano kitongoji cha Nambalapi na kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na fedha za BOOST katika shule mpya ya mkondo mmoja shule ya Msingi Nambalapi ambapo katika shule hiyo ilipokea jumla ya shilingi 331,600,000 kwaajili ya ujenzi wa madarasa 7 ya Shule ya Msingi, vyoo, jengo la Madarasa mawili ya awali ya Mfano na jengo la utawala. Na mpaka kamati inafika kwenye mradi huo mradi upo kwenye hatua za ukamilishaji.

Ambapo katika taarifa iliyosomwa na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo mbele ya Mwenyekiti wa Halmashuri wameweza kumshukuru Mhe Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwatengea kiasi hicho cha fedha, pia wameshukuru, Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mhe Jenista Joakim Mhagama kwa namna anavyolipambania Jimbo lake, pia wamekishukuru Chama cha Mapinduzi kwa kutekeleza ilani ya Chama , pia wamemshukuru Mwenyekiti wa Halmashuri pamoja na baraza la Madiwani kwa kuona umuhimu wa ujenzi wa shule hiyo kwani wanafunnzi walikuwa wakisafiri umbali mrefu kwaajili ya kwenda kusoma jambo ambalo lilikuwa linahatarisha usalama wa wanafunnzi

Kisha Mwenyekiti wa Halmashuri ametoa wito kwa vijiji vyote vya Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuhakikisha wanakuwa na akiba ya tofali ili kurahisisha ukamilishaji wa miradi pindi inapoelekezwa kwenye vijiji vyao kwani baadhi ya miradi imechelewa kukamilika kutokana na uhaba wa matofali katika vijiji husika

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa