• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

UJENZI WA MADARASA YA AWALI YA MFANO KATIKA SHULE YA MSINGI NDILIMA WAPAMBA MOTO

Tarehe ya Kuwekwa: September 7th, 2023


Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Songea, inatarajia kuanza ujenzi wa Madarasa mawili ya Awali ya Mfano kupitia Mpango LANNES yenye thamani ya shilingi Milioni 57,825,000.00katika shule ya Msingi Ndilima, Ujenzi huo unatarajia kuanza rasmi tarehe 08/09/2023.

Awali kamati ya ujenzi  wa mradi huo wameweza kukutana katika ofisi  ya kata ya maposeni  tarehe  05/09/2023  ikiongozwa na  Mwakilishi wa Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mwl. Sothery Nchimbi ambaye ni Afisa Elimu Maalum idara ya Elimu Msingi ili kuzijengea uwezo Kamati za ujenzi kupitia Force Akaunti.

Ambapo katika maelezo yake Mwakilishi wa Afisa Elimu wa Msingi ambaye ni Afisa Elimu Maalum  Halmashauri ya Wilaya ya  Songea ameiomba Kamati ya ujenzi kuwa waaminifu na kushirikiana katika kufanikisha ujenzi wa Madarasa hayo.

" Tunafanya ujenzi kwa ajili ya kuwezesha watoto wetu na wajukuu wetu waweze kusoma katika mazingira mazuri kwa hiyo niwaombe ndugu wajumbe kufanya kutekeleza  ujenzi huu kwa uaminifu na kwa kuzingatia ubora na kwa kuangalia mstabali wa maisha ya watoto wetu ambao  ndio  watakao soma katika Madarasa hayo na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumetekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi katika uboreshaji Elimu ya Tanzania"

"Aidha namshukuru Mheshimiwa Rais, Daktari  Samiah Suluhu Hassan Rais wa  Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha kwa ajili ujenzi wa miundo mbinu ya Elimu katika wilaya ya Songea Aidha nawashauri kamati kuepuke kufanya kazi kiurafiki kwani tutakwamisha ujenzi,na kusababisha  kujenga chini ya kiwango au vinginevyo"

Pamoja na hayo Mwakilishi huyo wa Afisa Elimu alitoa nafasi  kwa wataalamu kutoka ofisi ya Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ili kutoa ufafanuzi wa  kitaalamu wa mambo yanayohusu ujenzi kwa lengo la  kufanikisha ujenzi huo, Maafiasa hao walikua na haya ya kusema-;

Raymond Joseph Afisa Manunuzi wa Halmashauri  ya  Wilaya ya Songea" Lengo la kushirikiana kamati hii pamoja na wajumbe tunahitaji kuweka uwazi wa mradi, lakini kama Afisa manunuzi nawashauri kamati ya mapokezi ya ujenzi huu kuwa na kitabu cha reja ambacho kitasaidia kuandika vifaa vyote vitakavyo nunuliwa sokoni na kutoka stoo kuelekea kwenye ujenzi ili kuepusha upotevu wa vifaa wakati wa ujenzi"

Sambamba na hilo ni vema tukapata bei za sokoni ili kuepuka gharama kubwa za vifaa vya ujenzi ambazo zitaweza kukwamisha ujenzi huu, tuepuke kununua vifaa kwa kufuata urafiki na tusisahau kutunza risiti za manunuzi ili kutunza kumbukumbu" Alisema Raymond Joseph, nae

Jacob Mchaki Mhandisi wa ujenzi na katibu wa kamati ya ujenzi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Songea Alisema "Ni muhimu kwa kamati ya ujenzi ikazingatia mambo yafuatayo ili kufanikisha ujenzi huu, kuainisha mahitaji ya ujenzi, kuandaa ripoti ya maendeleo ya mradi ( progress report),. Kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya mapokezi na kupokea, kujadili na kufanyia kazi ushauri wa wadau mbalimbali". Pia

Emmables Francis Afisa mazingira kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Songea Alisema "Nilazima kuwepo kwa ushirikishwaji wa jamii juu ya mradi huu ili kuepusha migogoro hususani ya maeneo, pia kuzingatia eneo la upatikanaji wa nyenzo za ujenzi hususani kokoto na mchanga ili kuepusha uharibifu wa mazingira, kabla ujenzi haujaanza lazima kuwepo na choo kwaajili ya kuwezesha mafundi kujisitiri na haja, eneo la kuweka taka ngumu ili kuepusha utupaji wa taka hovyo na kupeleka uchafuzi wa mazingira, pia kutunza uoto wa asili na mwisho kuangalia ustahimilivu wa udongo kama unaweza kubeba jengo lenye kiwango gani.

Ikumbukwe kwamba mradi huu wa ujenzi upo chini ya ilani ya chama cha mapinduzi katika kuboresha Elimu ya Tanzania ambapo fedha za mradi zilikabidhiwa mnamo Tarehe 8 September 2022 na ujenzi huo unatarajiwa utaanza mara moja baada ya kikao hiki.





Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa