• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

TARURA kutumia milioni 701 kujenga daraja mto Muhukuru

Tarehe ya Kuwekwa: December 24th, 2021

 Wakala wa barabara za Mjini na Vijijini kutumia Shilingi milioni 701 kujenga daraja kwenye mto Muhukuru katika Kata ya Muhukuru barabarani Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma.

Meneja wa TARURA wa Wilaya ya Songea Mhandisi John Ambrose amesema ujenzi wa daraja ulitakiwa uanze Januari 4,2021 kutokana na changamoto za mvua mradi ulianza kutekelezwa mwezi Julai na unatarajia kukamilika mapema Januari 2022

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Muhukuru barabarani Mhe. Manfred Mzuyu amesema ujenzi wa daraja hilo utatoa fursa kwa wananchi kufungua mtandao wa mawasiliano na biashara kutoka sehemu moja kwenda nyingine hata nchi jirani ya Msumbiji.

Mhe.Mzuyu amesema ujenzi wa daraja hilo pia utarahisisha upatikanaji wa  huduma za matibabu  ya upasuaji wa dharula kwa magonjwa ya kidoletumbo,mabusha,mshipangili na wenye uzazi pingamizi kwenye kituo cha afya cha Muhukuru Lilahi ambapo awali wananchi walikua wakipata tabu kufika kwenye kituo hicho.

Mzuyu ameongeza kwa kusema ujenzi wa daraja hilo utaimarisha usalama wa wanafunzi kuvuka kwa usalama hasa nyakati za masika kipindi ambacho mito mingi hujaa maji na kusababisha athari kwa wananchi na mali zao.

Mzuyu amesema mradi wa ujenzi huo ni kiunganishi cha Vijiji vitatu na Vitongoji vyake ambavyo ni Muhukuru barabarani,Mbiro na Mipeta kuelekea  Kata ya Kizuka na Vijiji vingine.

Awali akikagua utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mhe. Jenista Mhagama amemshukuru Rais wa awamu ya sita Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha ya kujenga daraja ambalo litaimarisha uchumi wa wananchi.

Mhe.Jenista amewataka wadau wa ujenzi wa mradi huo kukamilisha ujenzi kabla ya Januari 15, 2022 ili wananchi waanze kunufaika na huduma hiyo

Imeandaliwa na kuandikwa na 

Jacquelen Clavery

Songea DC.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa