• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

TAASISI ya MUMIVI yatoa mafunzo ya Upandaji miti na Utunzaji wa mazingira Songea DC.

Tarehe ya Kuwekwa: June 2nd, 2023

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe ambae amewakilishwa na Afisa Mipango Bw. Athuman Nyange amefungua semina ya mafunzo ya mradi wa Upandaji miti na Utunzaji wa Mazingira Songea Vijijini.

Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa CCM Wilaya na kuudhuriwa na wajumbe mbalimbali wakiwemo Walimu wa mazingira wa shule za msingi na wawakilishi yaani Mabalozi wasimamizi wa mazingira ngazi ya Kata na Vijiji.

Mafunzo hayo yaliratibiwa na Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali inayoitwa Muunganisho wa Ujasiriamali Mijini na Vijijini (MUMIVI) ambayo inajishughulisha na Upandaji miti Pamoja na Utunzaji wa mazingira katika ngazi ya jamii.

Akizungumza Kaimu Mkurugenzi katika mafunzo hayo amewahasa wajumbe waliodhuria mafunzo hayo Kwenda kutoa elimu kwa jamii juu ya upandaji miti na utunzaji wa mazingira kwani kiwango cha uharibifu wa mazingira kipo juu sana hivyo elimu itolewe mapema.

“Elimu mtakayoipata hapa ikawe chachu na muwe mabalozi wazuri kwa Kwenda kuwaelimisha wananchi juu ya upandaji miti na utunzaji wa mazingira”, amesisitiza Bw. Nyange.

Akizungumza Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Koyigila Kazuzi amesema lengo la Taasisi ya MUMIVI ni kuunganisha watumiaji wa kuni na mkaa kuwa na wajibu wa kurejesha miti iliyopotea na inayoendelea kupotea kwa kutoa elimu na mafunzo juu ya upandaji miti na kuitunza, hivyo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea wamedhamiria kuanzisha miradi hiyo kwa kupanda miche ya miti katika shule za msingi mbili katika kila Kata.

Ameongeza kuwa kama jamii itazingatia utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti na kuitunza hivyo watakuwa wametunza vyanzo vya maji na kuboresha mazingira kwa kiasi kikubwa hivyo vizazi vijavyo vitanufaika na uhifadhi huo.

Nae Afisa Misitu Wilaya ya Songea Zakayo Kaunda amesema Agizo la Serikali ni kila Halmashauri ihakikishe inapanda jumla ya miti Milioni 1,500,000 kwa mwaka hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Songea imefanikiwa kupanda miti Milioni 1,200,000 hadi sasa katika maeneo ya shule, hospitali na taasisi mbalimbali za Serikali.

Hata hivyo nae ameunga mkono jitihada za taasisi ya MUMIVI kwa kutoa mafunzo na elimu juu ya Upandaji miti na Utunzaji wa mazingira.

Pia Afisa Elimu maalumu Mwl. Sothery Nchimbi ambae pia ni mdau wa mazingira amewasisitiza walimu na wadau wote wa mazingira walioshiriki mafunzo hayo nao waende kutoa elimu hiyo kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla hili mafunzo hayo yaweze kuleta tija.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa