• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SONGEA DC yapanga mipango mikakati ya uwajibikaji wa mwekezaji kwa jamii

Tarehe ya Kuwekwa: October 20th, 2022

HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea imedhamiria kuandaa mipango shirikishi itakayotumiwa na Wawekezaji, Serikali ya kijiji na Halmashauri katika sekta ya Kilimo na Madini hususani makaa ya mawe.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mhe.Menas Komba katika kikao kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri Lundusi-Peramiho wakati akizungumza na kujenga uelewa kwa Wawekezaji juu ya uwajibikaji wa kampuni kwa jamii (CSR).

Amesema lengo la kuandaa mpango huu ni kuondoa migogoro isiyokuwa ya lazima na manung’uniko kati ya wawekezaji, Serikali ya kijiji na Halmashauri ya Wilaya.

‘’Nichukue nafasi hii kuwashukuru wawekezaji sisi kama Halmashauri tutafanya kazi na nyinyi kwa asilimia 100 hivyo basi tutaomba ushirikiano wenu na yale tunayokubaliana nayo yafuatwe’’, amesisitiza Mhe.Menas.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe amewataka wawekezaji kuwa wawazi na waweze kushirikisha wanajamii juu ya mradi wanaoutekeleza  hii itaongeza thamani ya wawekezaji kwenye jamii.

‘’Naomba kuwashauri wawekezaji wetu kuwa wawazi kama mnatoa Shilingi Milioni sita kwa kwaajili ya kutekeleza mradi basi yote itumike kwenye mradi kwa uaminifu na muweze kushirikisha wanajamii katika ununuzi wa vifaa, pia katika kuihudumia jamii kwa asilimia 0.07 muweze kusema ni Shilingi ngapi kutoka kwenye jumla ya mauzo yenu’’, amesisitiza Ndugu Neema.

Akisoma taarifa Afisa Mazingira Makisio Chengula amesema kampuni ambazo zimekusudiwa katika mpango huu zipo sita ambazo ni Rutanza Coal Limited, AVIV Tanzania Limited, Agnes and Michael, Synergy Tanzania Company Limited, Com Coal Limited na Tuteikwa Investmant Company Limited.

Amesema mpango huu utazisaidia Serikali za vijiji kutambua miradi inayotekelezwa kwenye kata na vijiji vyao kupitia mwekezaji na itasaidia kijiji kuwa na mpango na kampuni husika.

Wakizungumza wawekezaji wameunga mkono mikakati iliyowekwa na Halmashauri, pia wamekubali kukaa pamoja na Halmashauri na kuweka mikakati juu ya kutekeleza uwajibikaji wao kwa jamii.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa