• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SONGEA DC WAKABIDHIWA VIFAA VYA MICHEZO

Tarehe ya Kuwekwa: September 14th, 2023

Watumishi wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea ambao pia ni wadau wa michezo wamepokea mipira 6 ya michezo kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kuboresha kuimarisha michezo na miili yao kwa kufanya mazoezi

Akithibitisha kupokea mipira hiyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Ndug.Makisio Chengula amekabidhi mipira hiyo na kuishukuru Serikali kuu kupitia ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma na kusema kwamba wamepokea mipira sita ambayo;- mipira 2 ya kikapu, 2 ya Pete na 2 ya miguu.. Ambapo amesema

" Nashukuru kwa muitikio wenu kama nilivyo waita, nimeona nichukue jukumu hili kubwa nitoe taarifa kwenu kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Songea imepokea mipira 6  lengo kubwa ni , kuboresha na kuinua michezo katika Halmashauri yetu,hivyo nimewaita ninyi kwaajili ya kuwakabidhi mipira hiyo pia kutoa hamasa ya michezo. Kwahiyo kama Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa umetukabidhi mipira ya michezo ikiwa miwili ni ya miguu, miwili ya netball na miwili ya basketball"

Ndipo alipotoa wito kwa watumishi wa Halmashauri ya Songea kwa kuwataka mipira hiyo wakaitumie  kama chachu ya ushirikiano mwema kati ya Halmashauri na vijiji vyote vinavyopatikana katika Halmashauri hiyo.

"Mipira hii Kwa kuwa tunawakabidhi ninyi Leo tunaomba mambo yafuatayo yakazingatiwe La kwanza Kwa kuwa Halmashauri yetu Bado ipo chini katika masuala ya michezo tunaomba wadau wote tuweze kushirikiana, tukiwa tunamaanisha sisi kama Halmashauri tunazo Kata mbalimbali pamoja na vijiji 56 tunaomba basi hii Iwe chachu kwenye Halmashauri yetu lakini nyinyi kama wadau wa michezo Bado mnanafasi ya kuitawanya na kuisambaza katika Halmashauri yote ya Wilaya ya Songea kwa kufanya michezo katika maeneo hayo.Jambo jingine najua ninyi ni watumishi na mnaratiba nyingi za shughuli mbalimbali za maendeleo hivyo pangilieni ratiba zenu vizuri ambayo itawawezesha kufanya kazi zenu na kupata nafasi ya kushiriki kufanya mazoezi" Alisema Makisio Chengula Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea

Nae Meneja wa timu ya Songea DC fc Hussein Hamidu akipokea mipira hiyo ameweza kuwashukuru wote waliohusika na msaada huo ikiwemo Serikali kuu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea kwa kuwakabidhi mipira hiyo ambapo amesema

"Binafsi kwaniaba ya timu ya Songea DC fc tunamshukuru sana Kaimu Mkurugenzi kwa kutukabidhi mipira hii ambayo  itatuwezesha kuendeleza michezo katika ngazi ya Halmashauri na kushiriki mashindano mbalimbali kuanzia ngazi ya Halmashauri, Wilaya Hadi Taifa, kipekee tunakupongeza wewe pamoja na  viongozi wengine wa Serikali kwa kuendeleza michezo mbalimbali, na hamasa kwa watumishi wa ngazi zote, kwa namna ya kipekee napenda kumshukuru Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mhe. Jenista Joakim Mhagama kwa kutupatia jezi ambazo zitatusaidia kuimarisha michezo, pia napenda kumshukuru Mwenyekiti wa Halmashuri kwa jitihada zake na kuipambania Halmashauri Aidha katika masuala ya michezo, pia Mhe.Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jitihada zake  kwa kutoa hamasa kwa watumishi kupenda michezo.

"Mwisho  tunapenda kuwaahidi kufanya vyema katika mashindano mbalimbali ikiwemo Samia Cup pamoja na mashindano ya Serikali za mitaa ambayo yanatarijiwa kuanzaTarehe 18 octoba  na ili kuwezesha hayo sisi kama watumishi wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea tumejiandaa kwa kujiimariaha kimazoezi, hivyo tunaomba wadau mbalimbali wa michezo kutupa ushirikiano kwa asilimia miamoja Alisema Hussein Hamidu Meneja wa Songea dc fc

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa