• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA PERAMIHO, AKUTANA NA WADAU WA VYAMA VYA SIASA KWA MAANDALIZI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA.

Tarehe ya Kuwekwa: October 18th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Peramiho, Bi Elizabeth Gumbo, amefanya kikao na wadau wa vyama vya siasa kutoka Halmashauri hiyo, kwa lengo la kujadili maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Katika kikao hicho, Bi Gumbo aliwataka viongozi wa vyama hivyo kuwa watulivu kuelekea uchaguzi huo, ili kuhakikisha unafanyika kwa haki, amani, na utulivu.

Akiwaeleza wajumbe wa kikao hicho, Bi Gumbo alifafanua kuwa idadi ya vitongoji katika wilaya hiyo itabaki ileile, ambayo ni 443, huku mabadiliko pekee yakiwa ni ongezeko la vituo vya kujiandikisha na kupigia kura, ambavyo sasa vimefikia 453. Alisema lengo la kuongeza vituo hivyo ni kurahisisha huduma kwa wananchi, ili wasilazimike kutembea umbali mrefu, akisisitiza kuwa vituo hivyo havina sifa ya kuwa vitongoji kwa kuwa vigezo maalum vya uanzishaji wa kitongoji havijatimia.


Aidha, Bi Gumbo aliwasihi wajumbe wa kikao hicho kutumia nafasi zao kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. “Zimebaki siku mbili tu za kujiandikisha. Nyinyi ndio wenye dhamana ya kuhamasisha watu wenu waliopo chini. Niwaombe sana, kwa muda huu uliobaki, mkawe mabalozi wa kuwahimiza wananchi kujiandikisha ili waweze kupata haki yao ya kikatiba ya kumchagua kiongozi anayewafaa,” alieleza Bi Gumbo.

Bi Gumbo alibainisha kuwa kwa mujibu wa kanuni na taratibu zilizopo, uongozi wa sasa utamalizika rasmi kesho, Oktoba 19, 2024. “Ni nafasi yenu sasa kuwaandaa wagombea kutoka kwenye vyama vyenu, kwani viongozi waliopo madarakani watamaliza muda wao rasmi kesho. Zoezi la uchukuaji wa fomu za kugombea nafasi mbalimbali litaanza rasmi Oktoba 26 hadi Novemba 1, 2024. Ni muhimu kufahamu kuwa fomu hizo zitatolewa tu kwa watu wenye barua ya utambulisho kutoka kwenye vyama husika,” alisisitiza.

Kwa upande wao, wajumbe wa kikao hicho walimshukuru Mkurugenzi kwa ushirikiano aliowaonyesha, huku wakimwomba aendelee kusimamia kwa umakini zoezi hilo ili uchaguzi ufanyike kwa amani, utulivu, na haki kwa kila mwanachama. Waliahidi kuwa watatekeleza wajibu wao wa kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato mzima wa uchaguzi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa